Ninaendelea vizuri. Ilikuwa ajali mbaya sana. Namshukuru Allah kwa kutuponya. Shukran Wahudumu wa Kituo cha Afya Kalya, licha ya changamoto, Huduma ya kwanza imetusaidia. Shukran Madaktari na Wahudumu Hospitali ya Maweni Kigoma. Mimi na wenzangu, mpaka sasa, ni wazima
Nimeruhusiwa kutoka hospitali. Nawashukuru madaktari na wauguzi Kituo cha Afya Kalya - Uvinza, Hospitali ya Maweni Kigoma na Hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam. Asanteni sana wote kwa Dua, Sala na maombi yenu. Nataraji kurudi kwenye kampeni siku chache zijazo In Sha Allah
Nimezunguka Nchi yetu na kuona hisia za Watanzania. Juzi Mtwara Mjini alinifuata mama mtu mzima sana na kuniambia “mwanangu mmeshindwa kukubaliana Mgombea mmoja? Tafadhali mwanangu jitahidini”. Nilipata uchungu sana moyoni. Watanzania wanataka MABADILIKO. TUNAWAPA
Nilipoamka leo nilikutana na ujumbe wa Simu “tutakushughulia labda usirudi”. Nikajisemea lipi jipya watafanya? Azory, Saanane na Kanguye wamewapoteza. Lissu wamemshambulia kwa Risasi ili kumwua. Erick na kina Tito wapo jela. Lipi lipya watafanya?
@MagufuliJP
SIKUOGOPI aslani
Ewe Mwanachama, mfuasi na mpenzi wa Chama cha
@ACTwazalendo
kura ya Urais wa Jamhuri ya Muungano ni kwa Tundu Lissu
@TunduALissu
. Huu ni wakati wa Mabadiliko. Tusigawe kura zetu wapinzani. Mimi nitampigia kura Tundu Lissu awe Rais wangu
Rais aliyepata sifa kubwa kwa kuondoa Wafanyakazi hewa katika utumishj wa Umma Amekubali ‘kuchaguliwa’ kuwa Rais kwa kutumia Kura hewa. Anawashukuru wapiga kura hewa kwa kumchagua huku akijua ushindi wake ni hewa. Ama kweli kua uyaone! Ukistaajabu ya Mussa utaona ya Furauni...
Watumishi wa Umma wameanza kupandishwa madaraja tangu wiki iliyopita na pia wanalipwa pesa zao. Nawaambia Watumishi wa Umma kuwa hayo ni matunda ya Kazi yetu wanasiasa wa Upinzani kuwasemea. Nawasihi sana watupigie kura nyingi ili tuunde Serikali itakayoheshimu Utumishi wa Umma
Kigoma Leo imewakusanya Lissu na Magufuli! Kuna mmoja kajiongezea shughuli ya Kiserikali ili akae kae Lwama. Lakini atakimbia Mji bila kuombwa! Mziki wa MABADILIKO Kigoma ni mnene mno.
Nimepata kusikiliza hotuba za kuvunja Bunge kadhaa, 2005 Rais Mkapa. 2010 Rais Kikwete na 2015 Rais Kikwete. Hotuba ya Rais Magufuli ya Leo inashangaza kidogo. Ilikuwa Kampeni zaidi. Ilikuwa hotuba ya kutazama nyuma na sio kwenda mbele. Ni Hotuba ya Rais anayemaliza muda wake
Tundu Lissu, karibu nyumbani. Umati uliokupokea ni ishara ya mapenzi makubwa kwako na shukrani kwa Mola. Sisi Viongozi wa
@ACTwazalendo
na wenzako wa
@ChademaTz
tunahikikisha tutakuwa na ushirikiano madhubuti ili kuleta MABADILIKO. Kurejea kwako ni chachu. Ni Furaha kubwa kwetu.
Watanzania tunapaswa kuamua. Kuamua kati ya kukumbatia UKWELI au UONGO. Kati ya HAKI na UKANDAMIZWAJI. Maamuzi sio kuhusu CCM au Upinzani, la hasha. Ni maamuzi kati ya kuwa na Nchi ya kidemokrasia au ya kidikteta. Ni lazima sasa kuisaka DEMOKRASIA
Matokeo yangu niliyokusanya Jimbo la Kigoma Mjini yanaonyesha kuwa nimeshinda Ubunge kwa kura 5218 licha ya maelfu ya Kura bandia. Lakini HAWATANITANGAZA! Wananchi wa Kigoma watakachoamua ndicho nitakachofuata
Siku ya 3 mfululizo naingia naingia ofisini nikiwa nimevaa Jezi ya
@SimbaSCTanzania
na ndio siku ambazo ufanisi kazini umekuwa mkubwa kuliko wakati wowote ule. Huu Uzi ni hatareeeeeeeeee
Watanzania hakuna wakati nafasi ni nzuri zaidi ya kuing’oa CCM kama wakati huu. Simameni Imara. Ukiona Chama tawala kime surrender shughuli za Siasa kwa Usalama wa Taifa jua Chama hicho kimekwisha hakipo. Watanzania kazeni kazeni
Jumatatu ya 27/7/2020 ni Siku muhimu sana Tanzania. Tundu A M Lissu aliondoka Dar kwenda Dodoma mapema Septemba 2017 akiwa kwenye Gari mzima. Aliondoka Dodoma kwenda Nairobi na kisha Ubelgiji akiwa mahututi baada ya kushambuliwa kwa Risasi 7/9/2017. Anarudi Dar akiwa Mzima.
Ni Leo au sahau demokrasia Tanzania. Twende kuandamana. Ni Haki ya kikatiba kuandamana. Madai yetu ya Uchaguzi kurudiwa na Tume Huru ya Uchaguzi ni madai halali. Twende tukalaani uvamizi uliofanywa Zanzibar na mateso dhidi ya raia ikiwemo mauaji. Wachache tutaumia WENGI watapona
Kiongozi mwengine amekamatwa jioni hii, Tundu Lissu. Najua ninafuata. Lakini nataka Umma ujue kuwa ninaamini kwa dhati Magufuli hakuchaguliwa kihalali katika Uchaguzi na Njia pekee ya kupambana na hilo ni maandamano ya Amani. Sisi ni waumini wa maandamano ya Amani! TUTASHINDA
Polisi walivamia Ofisi za
@ACTwazalendo
Kata ya Vingunguti ili kutukamata Mimi na Viongozi wenzangu. Nawashukuru Wananchi na Wanachama wetu waliozuia nisikamatwe. Ni maandamano ya AMANI yasiyo kikomo hivyo tutaendelea kuandamana mpaka madai yetu ya msingi yatekelezwe.
Moja ya sifa ya Kigoma ni Biashara ya vitenge. Baba yangu Mzee Kabwe amekuwa akifanya Biashara hii kwa miaka 30 sasa. Juzi nilimshikia duka wakati amepata dharura na nikamrejeshea duka baada ya saa. Leo nimepita kumuaga kuwa nakwenda kazini Dodoma
Waziri Simbachawene na IGP Sirro, waelezeni ma OCD na ma RPC waache ku harass Wananchi kwa kisingizio cha msiba. Rais Samia amesema tusonge mbele, unamharibia kwa kamatakamata zenu. Acheni kila raia aomboleze kwa njia zake Mwenyewe. Hakika hizi kamata kamata ni SABOTAGE v Samia
Video ya Mwezi Septemba Mwaka 2019 nilipokwenda kumsabahi Tundu kwa mara ya mwisho kabla hajarejea nchini. Leo nimetamka rasmi kuwa nitampigia kura ya Urais wa JMT
Simba Sports Club, a symbol of unity,
Bringing fans together, creating a community.
Through victories and defeats, they stand tall,
Their passion for the game, never to fall.
@SimbaSCTanzania
Tanzania ya baada ya 28.10.2020 itakuwa ya tofauti sana. Watanzania tujiandae kwa MABADILIKO. It is no longer business as usual. Kaeni tayari kwa MAELEKEZO
Hii military occupation ya Zanzibar wiki ya mwisho ya Uchaguzi wala haitutishi. Tutawashinda na Serikali mtatoa na hao wanajeshi watapiga saluti kwa Viongozi waliochaguliwa na Wananchi
Licha ya kuingiza kwenye vituo kura zilizokwishapigwa zipatazo 15,850 ( kura 50 kila Kituo cha kupigia kura ) nimemshinda Mgombea wa CCM kwa kura 5218. Hata hivyo Mgombea wa CCM katangazwa mshindi kwa tofauti ya kura 7000. Tunafungua ukurasa Mpya wa mapambano ya demokrasia nchini
Asubuhi hii ninakwenda Kituo cha Polisi kuwajulia hali Viongozi wenzangu Freeman Mbowe, Godbless Lema na wengine waliokamatwa kutokana na maandamano ya Amani tuliyotangaza kupinga Uchaguzi feki.
Another leader of the opposition, Tundu Lissu arrested. For sure I will be with them soon. I want to make clear, I believe in this cause, Magufuli wasn’t legitimately elected and I believe in fully 100% peaceful protests. We are believers in non-violence. We shall WIN this too
Kwa uchungu mkubwa nawajulisha kuhusu msiba mkubwa tuliopata wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama na Mkt wa Kamati ya Maadili Maalim Abubakar Khamis Bakar. Tangu walipompigia risasi chini ya miguu usiku wa tarehe 28/10/2020 hakuwa Sawa mpaka umauti. Inna lillah waina ilaih raajiun
I have received the sad news of the death of President Mkapa, President of Tanzania 1995-2005. It is a big loss to Tanzanians. My condolences to the family, relatives and all Tanzanians.
#RIPMzeeMkapa
Nashukuru sana bado kuna Watanzania wenye kujali weledi ( professionalism ) kama huyu. Anajibu bila woga na kwa ufasaha mpaka Amiri Jeshi Mkuu anakosa maswali wala mifano ya kujenga hoja zake. Natumai Rais
@MagufuliJP
atakuwa amejifunza kusikiliza wataalamu
Mpango ni kuumiza Watu kesho kwenye maandamano. Wananchi MSIOGOPE. Kila mtu mwenye smart phone ahakikishe ana rekodi kila kitu kuanzia kesho. Hawawezi kutuua wote Lakini watakaobaki wawe na ushahidi wa wauaji. REKODI KILA KITU KWA KUTUMIA SIMU YAKO. Tutawashinda hawa
Hapa ni pale panapoitwa flyover ya Mfugale ( TAZARA ). Daraja hili lilitumia USD 65M. Limetatua tatizo gani? Mvua ikinyesha kama Jana ndio panakuwa hivi. Miradi mingi iliyotekelezwa na Serikali ya CCM ya Awamu ya 5 ni WHITE ELEPHANTS! Waste waste waste
Tanzania in full blown one party dictatorship. We shall resist this. I urge Tanzanians not recognize any authority coming out of these widespread rigging. I ask the international community NOT to recognize this Tanzanian election. Consequences for this must be huge! RESISTANCE
Mapigo mfululizo kwa Mwanasheria mahiri Fatma Karume kutoka kwa Kampuni yake na kutoka kwa Dola ni ishara kuwa Fatma anaogopwa. Ninaamini kuwa Fatma atakuwa Imara zaidi. Ninalaani vikali sana kumwondoa Fatma kwenye daftari la Mawakili. Yana mwisho Haya
Nimezungumza kwa Simu na Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama
@SuluhuSamia
kumpa pole ya msiba wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania
@MagufuliJP
kufuatia Taarifa Rasmi ya msiba huo kwa Taifa.
Nilipata kusema Uchaguzi wa Tanzania wa 2020 ni marudio ya Uchaguzi wa India 2004. BJP walijinadi kwa SHINING INDIA wakati Umasikini unatamalaki Vijijini. Wananchi wakatoa Ushindi kwa Congress. Maamuzi ya Watanzania Oktoba 28,2020 yatawaacha watawala midomo wazi! INDIA 2004!
Naibu Katibu Mkuu wa Chama
@ACTwazalendo
ndg. Nassor Mazrui AMETEKWA na wanaosemekana kuwa Vijana wa Jeshi la JKU Zanzibar asubuhi ya Leo. Nazitaka Mamlaka za Zanzibar kumwachilia mara moja Mazrui. Huu ni uchokozi uliovuka mpaka
“Ndani ya siku 18 za Urais wa Samia Suluhu, nchi imejawa na FURAHA, siyo kwamba amepandisha mishahara (HAPANA), siyo kwamba ameajiri (HAPANA) siyo kwamba anagawa pesa huko mitaani (HAPANA) bali ni MATAMSHI yake tu kama [...] yanaendelea kuliponya Taifa bila sindano wala vidonge”
First Hijab wearing woman to become a President of a country in Africa with Bishops and Arch-Bishops of Tanzania Episcopal Conference. This is Tanzania! The state of our own creation. Whatever the difficulties, Tanzania shall remain ONE, Strong and UNITED.
“Mkuu wa mkoa wa LINDI Bwana Geofrey Zambi jioni ya Leo katishia kuvunja miguu waandamanaji.” Tunaweka rekodi ya maneno Haya. Hata sisimizi akivunjwa mguu yeye huyo Zambi atawajibika....
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Ismail Jussa amefika Nairobi kwa matibabu zaidi baada ya kuumizwa vibaya kwa kipigo akiwa mikononi mwa polisi na vyombo vya Usalama Zanzibar. Jussa aliumizwa sana. Mungu atamsaidia
Nilivyomwelewa Rais
@SuluhuSamia
leo
1.Tumalize Miradi yote ya kimkakati inayoendelea
2.Tuimarishe Taasisi za utoaji Haki kwa Wananchi na Wawekezaji
3.Tujielekeze kukuza uchumi wa Mwananchi mmoja mmoja kwa kuongeza mzunguko wa Fedha
Basi Rais asiongee tena Mwaka mzima!
Polisi Lindi, tunajua mnachomfanya Dkt. Mmoto Mgombea Ubunge wa Upinzani Jimbo la Nachingwea. Mnampa makosa ya Ugaidi na mnamtesa. RPC Lindi acheni kabisa huu unyama mnaoufanya. Tanzania inaona, Dunia inaona. RC Lindi Bwana Zambi tunakuongeza katika orodha ya ICC.
@MariaSTsehai
Kwa Wananchi wa Tanzania na haswa Wananchi wa Kigoma Mjini, Hii ni sura mpya ya udikteta nchini. Tusikate Tamaa. Tutapambana kwa namna ambayo Tanzania itakuwa tofauti sana.
#Zambia
President
@EdgarCLungu
has conceded in a letter sent to now president elect
@HHichilema
of
@UPNDZM
. Once again Zambia has shown the world the level of its democratic maturity. Peaceful transfer of power is happening for third time in history. Congratulations Zambians
Kituo cha kupigia kura Shule ya Msingi Airport, Afisa Usalama wa Wilaya ya Kigoma na Tume ya Uchaguzi ndipo wanapanga kufanya mabadiliko ya Matokeo kwa kutumia kura za bandia. Vituo vyote katika Kata ambazo ACT inaongoza fomu za Matokeo hazitolewi. Tunapambana
Katika Jimbo langu kura wapiga kura hewa 13,830. Wameongezwa kwenye daftari la wapiga kura. Kura zao zitapigwa na 1) Askari wa JKT na 2) Wanafunzi walioandaliwa. Nataka kumwambia Mkuu wa Usalama wa Taifa Diwani Athumani kuwa kwa Kigoma Mjini atakachokipata ATAJUTA! Awalete tu hao
Mimi nipo tayari kuwa shahidi wa mapambano ya kutaka demokrasia Tanzania. Kesho 2/11/2020 nitaandamana kwa Amani kutaka
⁃Uchaguzi Mpya
⁃Tume Huru ya Uchaguzi
⁃Kulaani mauaji ya raia, utekaji wa Nassor Mazrui na wengine na uvamizi wa kijeshi Zanzibar
#Nitaandamana
Alipokuwa Bunda alisema hawana Taa kwa sababu walichagua Upinzani. Alipokuwa Busega ( Lamadi ) akasema mkichagua Upinzani hataleta Maendeleo. Alipofika Kigoma akasema Haya Maendeleo Haya ni yangu nimeleta, Maendeleo hayana Vyama🤣🤣! Ni kauli za Mtu mmoja katika Uchaguzi mmoja!
Mpango wa Kura bandia kwa Jimbo langu ilikuwa kura 15,000+! Tumefanikiwa kudhibiti kwa kiwango kikubwa. Lakini bado kuna kazi kubwa sana. CCM hawana aibu kabisa! Ni wanyama. Kigoma itawaka moto
Tumefika salama Toronto, Canada. Tunaendelea na ziara yetu ya kimataifa, kuonana na Watanzania wanaoishi nje ( diaspora) na kuzungumza na Serikali za Nchi hizo na Taasisi za Kimataifa ili kuhakikisha kuwa Uchaguzi wa Tanzania unakuwa Huru, wa Haki na unaoaminika ( credible)
As Tanzanians, we face a choice. The choice between truth and lies, between justice and injustice. The choice is not about CCM or the opposition. The choice is between democracy and autocracy. Democracy is demanded not supplied. For that we must take ACTION.....
Leo nimeshiriki mazishi ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kijijini kwake Lupaso - Masasi Mkoa wa Mtwara. Kuna mambo kadhaa ambayo binafsi sikukubaliana na Rais Mkapa, Lakini kama ilivyo kwa Nyerere, Mwinyi na Kikwete, hakutumia nafasi yake kupendelea Wilaya yake kimaendeleo
Leo, na Saa hii, imetimia miaka 6 tangu Mama yetu mzazi Hajjat Shida Salum Mohamed atangulie mbele ya Haki. Mwenyezi Mungu aendelee kutujaalia nguvu za kuvuka mitihani na Mola akubali Dua zetu na Istighfar kwa mzazi wetu.
Tunasikia kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) haitateua baadhi ya wagombea kutoka Vyama vya Upinzani katika nafasi ya Urais na Ubunge kwa sababu mbalimbali za kubumba. Namtahadharisha Jaji Kaijage asikubali kuhalalisha mpango huo dhalimu vinginevyo HAPATAKUWA na UCHAGUZI
#Umma
Mgombea Urais wa CCM alipokuwa Kigoma juzi alisema kuwa yeye ndiye alimtuma Waziri Mkuu Majaliwa kuanzisha Mradi wa kufufua zao la Michikichi Kigoma. Leo nitakuwa Mwandiga na nitawaonyesha kwa ushahidi chanzo cha Mradi huo na kwamba Magufuli HAHUSIKI kwa LOLOTE! Anadikiria mambo
Ibara ya 13(6)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatamka “ ni MARUFUKU kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazomtweza au kumdhalilisha”. Yaani torture is STRICTLY PROHIBITED in Tanzania. Simulizi za mateso zinazoendelea Mahakamani zinaumiza sana
Matokeo ya Kigoma Mjini bado kutangazwa. Lakini SITATANGAZWA. Kwa hiyo Watu kwa sasa tuchukue hatua zinazofuata. Hata wakiamua kunitangaza hayana Maana kwangu. Demokrasia ya Tanzania ina Maana zaidi kuliko Jimbo moja la Kigoma Mjini
Mola akijaalia umri na kuwa na mamlaka, hata Sirro akiwa amestaafu yupo kijijini, nitamteua tena kuwa IGP ili nimfukuze kazi. Rekodi yake iwe kufukuzwa na kushtakiwa na sio kustaafu. Amewafanya Watanzania wote Watoto leo
It was a very bad accident. I am ok. My colleagues including our candidate for Kigoma South and party officials are better too. Admitted at Maweni hospital in Kigoma for further transfer
Ninatamani kufanya Mdahalo na Rais
@MagufuliJP
kuhusu hali ya Maendeleo ya Nchi yetu kwa kutumia takwimu zinazotolewa na Mamlaka za Serikali yake mwenyewe. Nadhani Watanzania wanastahili mdahalo huo wakati wa Uchaguzi 2020
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania
@tanpol
unawezaje kukubali Kituo cha Polisi kutumika na genge la watekaji? Unajisikiaje raia ambaye anapaswa kujiona salama kituoni akiteswa kutoka kituoni? Unawezaje kukubali Jeshi hili? Kamanda Wambura nakuomba 1) Ufanyike uchunguzi HURU wa kina
#Video
Edger Mwakalebela maarufu kama Sativa ambae anadaiwa kutekwa Dar es Salaam siku chache zilizopita amesema baada ya kutekwa alipelekwa kituo cha OysterBay.
Sativa ameyasema hayo wakati akiwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mpimbwe alipokuwa akipatiwa matibabu kabla ya
Mimi ni Mbunge wa Kigoma Mjini. Nipo Dar es Salaam. Sijakwenda Dodoma Bungeni Kwa sababu ninaamini kuwa Bunge lilipaswa kuahirishwa ili kupambana na Korona. Sitakwenda Dodoma. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam hana Mamlaka yeyote ya kuniamulia niwe wapi katika Jamhuri ya Muungano
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo May 06 ametoa Saa 24 kwa Wabunge wote waliogoma kushiriki vikao vya Bunge na kwenda DSM kuhakikisha wanarudi Bungeni tofauti na hapo watakamatwa kwa kosa la Uzururaji.
Maandamano yetu kesho tarehe 2/11/2020 yatakuwa ya Amani. Wanachama na wafuasi wetu wanajua Hilo: MAANDAMANO YA AMANI. Tuna mashaka kuwa Polisi wataua Watu. Tunawaonya kuwa wauaji watawajibishwa binafsi. Tunataka Uchaguzi mpya chini ya Tume mpya ya Uchaguzi
Shambulio dhidi ya
@freemanmbowetz
Mwenyekiti wa
@ChademaTz
linashtusha na kukasirisha. Natoa pole kwa familia ya Mbowe, wanachama wa CHADEMA na Watanzania. Vyombo vya uchunguzi vinapaswa kufanya uchunguzi wa kina dhidi ya matukio ya kinyama kama haya.
Mwenyekiti wa Jimbo la Kigoma Mjini Bwana Suleiman Simba amekamatwa na Polisi Kituo cha kupigia kura cha Stendi Mpya kata ya Kasingirima, alikuwa anazuia kura ZILIZOKWISHAPIGWA kuingizwa Kituoni. Usalama wa Taifa ndio wanafanya kazi hiyo
Rais
@MagufuliJP
kakusanya marais wastaafu huko Chamwino. Nimetazama picha wote hawajavaa Barakoa. Wote 3 ni watu wazima sana walio hatarini mno kuathiriwa na Korona. Juzi Rais
@jmkikwete
alikuwa na Barakoa, Leo kaiacha. Mkapa pia. Mzee Mwinyi (
@Dullahmwinyi1
??? ) pia. SIO SAWA
Tupo tayari kwa Uchaguzi. Kwa upande wa majimbo tumeona tunaokwenda kushindana nao. Kwa Kigoma nimesikitika kuwa sauti muhimu kama Nsanzugwanko, Serukamba na Hasna hawatakuwapo Bunge la 12. Kwa Nchi uzoefu wa Mzee Chenge tutaukosa hasa kipindi hiki watu wanataka kubadili Katiba.
Mauaji ya raia Zanzibar hayatapita kimya. Mashahidi hawa wa ukombozi wataenziwa daima. Uchunguzi wa Kimataifa utafanyika na wauaji kuchukuliwa hatua. Kesho tupige kura kwa wingi sana Kwa Wabunge, Wawakilishi wa Upinzani, Rais Lissu na Rais Maalim Seif