The Guardian Ltd
Home of Great Newspapers
Mikocheni Light Industrial Area
P.O. Box 31042
Dar es salaam
Tel:+255 745 700 710
customerrelations
@guardian
.co.tz
📢📢📢 OFA OFA OFA
Kwa wasomaji wetu
Je unataka kusoma gazeti lako la Nipashe au The Guardian BURE mtandaoni? Basi fanya yafuatayo
Comment neno “Nipashe” katika kurasa za Nipashe (
@NipasheTz
) kwa Facebook na Instagram, na utapokea maelekezo DM namna gani utaweza kujisomea
#HABARI
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Albert Chalamila amesema kuwa anaunga mkono mabadiliko ya Katiba Mpya akieleza, Katiba ya sasa inasema Rais akifa Makamo ndiye anakua Rais, amedai inawezekana akapatikana Makamu wa Rais mchawi akamroga Rais ili yeye awe Rais wa nchi.
#HABARI
BAADHI ya wanafunzi wa udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Tiba, Sayansi na na Teknolojia (UMST) cha Khartoum, wamefurahishwa na mapokezi waliyoyapata Tanzania na kueleza kuwa ni matarajio yao kuwa watamaliza masomo yao ya vitendo salama./
#Video
Edger Mwakalebela maarufu kama Sativa ambae anadaiwa kutekwa Dar es Salaam siku chache zilizopita amesema baada ya kutekwa alipelekwa kituo cha OysterBay.
Sativa ameyasema hayo wakati akiwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mpimbwe alipokuwa akipatiwa matibabu kabla ya
#HABARI
MWANAFUNZI wa kidato cha nne Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST), Madeleine Kimario, amechangisha Sh. milioni 100 kwa ajili ya kusaidia mazoezi tiba kwa watoto wenye tatizo la usonji.
#HABARI
BAADHI ya wasomi, wazazi na wadau wa elimu nchini wameeleza mtazamo wao kuhusu wimbi la sasa la wahitimu wengi wa kidato cha nne, kuachana na masomo ya kidato cha tano na kutimkia vyuo vya kati kusomea fani mbalimbali. /
#NUKUU
“Mimi sijawahi kuwa na mkwe anaitwa
@zittokabwe
wao wanafanya starehe zao kichakani huko wanaendelea, sina mkwe anawezwa kuitwa hivyo na sitegemei kama atakuwa mkwe katika familia yangu." Abdallah Bulembo
#HABARI
KAPTENI wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Exavery Mroso (28) kutoka Kikosi cha Jeshi (603 KJ) cha Anga Kituo cha Banana,Dar es Salaam, amefikishwa mahakamani kwa madai ya kuingilia mfumo, kubadili neno la siri na kuwazuia viongozi kufanya kazi./
#HABARI
MSHAMBULIAJI wa Yanga, Fiston Mayele ameomba kuondoka kwenye kikosi hicho na kwenda kutafuta changamoto nyingine huku klabu ya Kaizer Chief ikatajwa kumtaka Mkongomani huyo. /
#MICHEZO
UONGOZI wa klabu ya Yanga wapo ‘kazini’ kusaka Kocha Mkuu wa timu hiyo baada ya kuondoka kwa Mtunisia, Nasreddine Nabi huku Mkongomani Florent Ibenge akipewa nafasi kubwa kutuwa kikoni hapo. /
#HABARI
WANANCHI wa kijiji cha Miyuguyu kata ya Kiloleli mkoani Shinyanga, wamechangishana na kutafuta nyumba kwa ajili ya mwalimu wa kike aliyejulikana kwa jina la Getrude Missana aliyekuwa anaishi katika ofisi moja iliyopo katika shule ya msingi Miyuguyu.
#HABARI
MAHAKAMA Kuu jijini Dar es Salaam, imeamuru mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya sheria katika Chuo Kikuu Tumaini Dar es Salaam (Tudarco), Mwajuma Malulu, kurudishwa chuoni baada ya kufukuzwa kwa madai ya kukiuka kanuni za mitihani. /
#MaandamanoCHADEMA
MZEE Gregory Gabone (69), akisubiri maandamano karibu na ofisi za Umoja wa Mataifa leo. Gabone ambaye ni Mwenyekiti wa wazee wa CHADEMA Mkoa wa Kagera, ametokea kijijini Bugene, Karagwe mkoani Kagera kushiriki maandamano hayo leo.
#HABARI
KIKOKOTOO cha mafao asilimia 33 kimeendelea kuwa mwiba huku wabunge wakihoji serikali kwa nini kikokotoo hicho hakifanani na kile kinachotumika Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Usalama wa Taifa./
#MICHEZO
KIUNGO wa Azam FC, Sospeter Bajana ambaye anatajwa kuwaniwa na Simba amesema kwamba yupo kwenye mazungumzo na timu zote mbili na anachoangalia ni maslahi zaidi. /
#HABARI
PURUKUSHANI za vuta nikuvute zimeibuka kati ya polisi na Wakili wa Kujitegemea, Baraka Mkama, katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya wakili huyo kuzuia askari kuwakamata wateja wake./
#HABARI
RAIS Samia Suluhu Hassan, amepiga marufuku uuzaji wa chakula nje ya nchi huku akiagiza kila Mtanzania kuhifadhi chakula, kwa ajili ya kukabiliana na uhaba wa chakula na mfumuko wa bei unaoendelea kupaa ulimwenguni kote. /
#NipasheBUNGENI
Kamati ya Maadili ya Bunge: Tulimuuliza CAG Assad kama ataacha kulitumia neno udhaifu akasisitiza ataendelea kulitumia na hakujutia kulitumia dhidi ya Bunge.
CAG hakuomba msamaha wala kujutia na akasisitiza ataendelea kulitumia neno hilo.
#NipasheMwangaWaJamii
#HABARI
Magari 7 yaliyojaza askari wenye silaha za moto, mabomu pamoja na mbwa yamezingira Ofisi za
@ChademaTz
Kanda ya Victoria jijini Mwanza kuzuia maombi ya kumuombea Mwenyekiti wa CHADEMA,
@freemanmbowetz
, yaliyopangwa kufanyika katika ofisi hizo./
“Embu jifikirie umenikamatia ng’ombe wangu 100, yani naona zinaenda sina uwezo wa kwenda Polisi kuna bunduki, haya nina kosa unazichukuwa ng’ombe zangu unaziuza mimi ninarudi masikini halafu baada ya miezi sita unaanza kunihudumia na fedha za Tasaf, hiyo ni akili gani jamani."
#CAGBUNGENI
Prof Assad: Hatujakurupuka kufanya mkutano huu hapa ofisini kwetu. Tulihisi mapema hatutakaribishwa bungeni. Tumeongea nanyi hapa kwetu, hata kama ninyi waandishi wa habari hamtatoa hiki tulichozungumza, sisi tutatoa kwa umma.
#NipasheMwangaWaJamii
#HABARI
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, Tundu Lissu, ameondoka nchini juzi kupitia mpaka wa Namanga kuelekea Nairobi, nchini Kenya, ambako alianza rasmi safari ya kwenda katika mataifa ya Ubelgiji na Marekani.
Lissu, atakaa nje ya nchi kwa
#HABARI
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Mbunge Mbogwe, Nicodemus Maganga, kama anataka kuhudumia wananchi afuate utaratibu wa nchi na akitaka kulipwa kwa dola ahamie katika nchi zinazofanya hivyo.
#HABARI
JESHI la Polisi mkoani Arusha, linamshikia Blandina Fred mkazi wa Kijiji cha IIkirev, Kata ya Olturoto wilayani Arumeru, kwa tuhuma za kumuua kwa kumchoma kisu mpangaji mwenzake, Erick Adam kisa shilingi 1000 ya mchango wa umeme. /
#NipasheJumapili
JESHI la Polisi mkoani Mwanza linatarajia kumfikisha mahakamani Mbunge wa Nzega Vijijini (CCM), Dk. Hamis Kigwangalla kwa tuhuma za kumpiga na kumjeruhi mlinzi wake, Jumanne Omary (66). /
#HABARI
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema chama hicho hakiko tayari kwenda kwenye uchaguzi mkuu bila Katiba mpya, sheria mpya ya uchaguzi na Tume Huru ya Uchaguzi./
#HABARI
JESHI la Kujenga Taifa (JKT), limetangaza kuchukua wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita mwaka 2023 wa shule za Tanzania Bara kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria baada ya kuboresha miundombinu ya kambi zake./
#HABARI
ZAIDI ya walimu 200 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, mkoani Mara wamewasilisha katika ofisi ya Ofisa Utumishi Wilaya, barua za maombi ya kujiondoa katika Chama cha Walimu Tanzania (CWT) huku wengine 120 wakijiondoa katika chama hicho.../
#HABARI
RAIS Samia Suluhu Hassan amesema amepokea ripoti ya awali kuhusu hali ya mashirika ya umma, akimpa kazi ya mwisho Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, kumalizia tathmini ili achukue uamuzi mgumu. /
#HABARI
ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania Sweden, Wilbroad Slaa, amesema haoni sababu inayowezesha wabunge 19 wanaoongozwa na Halima Mdee kuendelea kuwapo bungeni ilihali chama chao kilishafanya uamuzi dhidi yao. /
#HABARI
MKUU wa Mkoa wa Mwanza Amos Makalla amemjia juu Mwenyekiti Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe juu ya kauli zake za ukosoaji katika sakata la Mkataba wa uwekezaji wa Bandari na kueleza kuwa hiyo ni hatua kubwa..../
#HABARI
BALOZI Willibrod Slaa ameunga mkono uwekezaji kwenye Bandari ya Dar es Salaam, lakini ameishauri Serikali kurekebisha kasoro zinazolalamikiwa kwenye mkataba wa uwekezaji na Kampuni ya DP World ya Dubai./
#HABARI
MWENYEKITI wa
@ChademaTz
,
@freemanmbowetz
leo ameifahamisha Mahakama kwamba wanakosa haki ya kula chakula wawapo Mahakamani (Ubungo) na gerezani kwa miezi mitano./
#MICHEZO
KOCHA Mkuu wa Simba, Robert Oliveira ‘Robertinho’, amesema mipango yake ni kuona Simba inafanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa na sasa anaumiza kichwa kuona namna gani anakiandaa kikosi chake kwa ajili ya michuano hiyo. /
#HABARI
DEREVA wa basi la Saratoga linalofanya safari kati ya Dar es Salaam na Kigoma, Yassin Shabani, amejeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Pwani, Tumbi, baada ya kupigwa na askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)./
#MICHEZO
LIONEL Messi amethibitisha kuwa “hafikirii” kama atacheza Kombe lingine la Dunia baada ya kuiongoza Argentina kutwaa ubingwa wa mashindano hayo mwaka jana nchini Qatar. /
#HABARI
Diwani wa Mbagala Kuu Shabani. Othman Abubakari (CCM), amefariki dunia katika moja ya nyumba ya kulala wageni iliyoyopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam.
#HABARI
DEREVA wa Gari la kubebea wagonjwa katika Hospitali Maalumu ya Magonjwa ambukizi ya Taifa Kibong’oto iliyopo wilayani Siha Aliru Tibiika, amelalamikia kitendo cha kupigwa makofi na Askari Polisi akimtuhumu kuwa alitaka kumgonga. /
#HABARI
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mpango wa kutoshiriki uchaguzi wa madiwani wa kata 14 zilizotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi./
#HABARI
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeelezwa kuwa Happiness Fredrick, aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kabla ya kunyongwa na anayedaiwa mpenzi wake, alimtumia mama yake ujumbe mfupi kwa simu wamuombee yupo kwenye wakati mgumu.
#HABARI
WAKILI wa Utetezi, Peter Kibatala katika kesi ya mauaji ya dada wa marehemu Erasto Msuya ‘Bilionea Msuya’, Aneth Msuya, amedai mahakamani wana taarifa aliyekuja kutoa ushahidi kama dada wa kazi wa marehemu si Getruda Mfuru, bali ni askari kutoka Zanzibar.
Alidai hayo
#TETESI
DILI la kiungo mshambuliaji wa Al Ahly, Luis Miquissone, kurejea klabu yake ya zamani, Simba kuelekea msimu mpya wa 2023/24, ni kama limefikia asilimia 80, lakini shida ni maslahi binafsi ya winga huyo hatari, imeelezwa./
#HABARI
ASKOFU Mkuu mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, ameishauri serikali kuwajengea uwezo wananchi, ili waendeleze miradi iliyopo nchini ukiwamo uendelezaji wa bandari kuliko kutegemea wawekezaji wa kigeni..
#HABARI
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imepokea kielelezo cha gari aina ya Landrover lenye namba za usajili T 429 BYY kinachohusishwa katika mauji ya mdogo wa marehemu Erasto Msuya, maarufu Bilionea Msuya, Aneth Msuya, baada ya gari hilo kuhifadhiwa../
#HABARI
WAJAWAZITO zaidi ya 2,000 wamejitokeza katika mbio za Mamathon zilizozinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, Jokate Mwegelo, kati yao saba walipata uchungu wakiwa katika mbio na kupelekwa hospitali./
#NipasheJumapili
SERIKALI imesema nchi tano zikiwamo China, Marekani na Uingereza zimeonyesha nia ya kuwekeza kwenye ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) ushoroba wa Mtwara kupitia ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP). /
#HABARI
MGOMO wa wafanyabiashara Kariakoo, jijini Dar es Salaam, umeingia siku ya pili huku baadhi wakisema wanasubiri kikao kitakachofanyika leo kati ya viongozi wao na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa,kwa ajili ya kutatua kero walizoziainisha kwa muda mrefu./
#MICHEZO
WINGA wa RS Berkane ya Morocco, Victorien Adebayor, amekubali kujiunga na klabu ya Simba kwa ajili ya msimu ujao wa ligi baada ya mazungumzo na viongozi wa klabu hiyo jijini Dar es Salaam. /
#NipasheJumapili
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amewataka wa Wananchi wa Kijiji cha Ng’ambi na vijiji jirani kuacha kuuza ardhi kwa wageni kwa sababu mradi wa umwagiliaji utawanufaisha kiuchumi./
#HABARI
WADAU wa elimu walioshiriki Kongamano la Sera na Mitaala ya Elimu, wametoa mapendekezo kadhaa ikiwamo kufuta mitihani ya kitaifa ya darasa la nne, la sita na kidato cha pili./
SWALI: Zipo taarifa kwamba hauko sawa na familia yako. Kuna ukweli upi katika hili daktari?
DK. SLAA: Nina watoto wawili na mama wa kwanza ambaye hatujafunga ndoa, Rose Kamili, ambao leo ni watu wazima. Baadaye nikafunga ndoa kule Canada na Josephine lakini tulikuwa...
#NipasheJumapili
RAIS Samia Suluhu Hassan, kesho Juni 12,2023 anatarajia kuanza ziara yake ya kikazi siku tatu mkoani Mwanza yenye lengo la kukagua maendeleo ya miradi ya kimkakati, kuzungumza na wananchi pamoja na kufungua Tamasha kubwa..../
#HABARI
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, amesema kuwa ataandika barua ya kuomba ridhaa ya chama chake kugombea kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajika kufanyika Mwezi Oktoba, Mwaka huu.
#HABARI
SERIKALI imeombwa kuchapisha noti mpya zenye picha ya aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dk. John Magufuli, kwa ajili ya kumbukumbu na kuenzi kazi nzuri alizolifanyia taifa wakati wa uhai na uongozi wake./
#HABARI
MAISHA mapya ya majeruhi wa ajali ya basi la mwendo wa haraka (mwendokasi) , Osam Milanzi, baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini, yamegeuka kitendawili kwa ndugu, jamaa na marafiki kutokana na kupoteza kumbukumbu.../
#HABARI
FAMILIA ya marehemu Nusura Hassan Abdallah, aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), imefunguka ikisema taarifa za kifo cha mtoto wao walizipata kutoka kwa mchumba wake, Juma Kundiya ambaye ni mwalimu wa sekondari iliyoko Marangu..../
#coronavirus
Msanii
@MwanaFA
amesema baada ya kufanya vipimo vya COVID-19 amekutwa na maambukizi ya virusi hivyo. Ameeleza kuwa Jumanne alirejea nchini akitokea Afrika Kusini akawa hajisikii vizuri ndio akachukua uamuzi wa kupima.
"Hatukuwa na chochote cha kupoteza, ndio maana mechi imekuwa kama ilivyokuwa ndio maana nikapanga wachezaji watakaoweza kukaba zaidi kuliko kushambulia, sikuwaweka Djuma Shabani na Lomalisa" -kocha wa
@yangasc1935
Nasredine Nabi.
#HABARI
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema pamoja na mvua zinazoendelea kunyesha lakini bado hazijasaidia kutoa kiwango cha juu cha maji kinachoweza kupata umeme wa uhakika./
#HABARI
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amesema kabla ya Uchaguzi Mkuu na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ujao, kuna haja kufanya kila linalowezekana kubadili katiba ili kuwaondoa walimu kuusimamia.
Amesema mabadiliko wanayoyataka
#NipasheJumapili
MKAGUZI wa Jeshi la Polisi, Ally Babu amefunga ndoa ya kijeshi na mchumba wake, Selani Sumai ambapo tukio hilo lilikuwa kivutio kwa wakazi wa Arusha na kwa walioshiriki kutokana na kufanyika kwa matukio mbalimbali ya kijeshi ikiwamo.../
#HABARI
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kinondoni imeiamrisha Hospitali ya Muhimbili kuwapima watuhumiwa watatu ambao ni Noel Ndale Mushi, Kelvin Maliki Ngao na David Brayan Johnson kama wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
#HABARI
Mufti wa Tanzania, Shekhe Aboubakar Zuber, ameziomba mamlaka zinazohusika na kesi inayowakabili viongozi wa Uamsho iharakishwe kusikilizwa ili hatima yao ijulikane.
#NipasheJumapili
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kesho Juni 19, 2023 ataanza ziara ya kikazi ya siku saba nchini Uingereza zikiwa zimepita wiki mbili tangu alipofanya ziara kama hiyo katika nchi za Italia na Ujerumani./
#BREAKINGNEWS
Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali ya Kairuki, Dar es Salaam.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa alipata changamoto ya kifua na kupelekwa alfajiri ya leo Hospitalini hapo na baadaye kufariki.
#HABARI
MBUNGE wa Ilala Azzan Zungu ametaka kuwepo na kodi ya uzalendo itakayokatwa katika mitandao ya simu kwa kila Mtanzania kwa siku kama chanzo kipya cha mapato kwa Serikali.
#Habari
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari
@Nnauye_Nape
amesema serikali ya Tanzania iliitaka kampuni ya Starlink inayomilikiwa na Elon Musk kuweka ofisi zake hapa nchini ili waweze kulinda data za watumiaji na kuwajibika kwa watanzania.
#NipasheMwangaWaJamii
#NipasheHabari
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Husein Mwinyi, amesema amani iliyopo nchini haitokani na ukubwa wa majeshi au wingi wa askari, ila inatokana na utulivu wa wananchi wenyewe.
#HABARI
WATUMISHI sita katika Halmashauri ya Mji Tunduma wilayani Momba wamefukuzwa kazi na wengine wawili kupewa adhabu ya kukatwa asilimia 15 ya mishahara yao kwa kipindi cha miaka mitatu baada ya kupatikana na makosa mbalimbali yakiwamo ya ubadhirifu. /
(𝐈𝐦𝐞𝐚𝐧𝐝𝐢𝐤𝐰𝐚 𝐍𝐚 𝐂𝐡𝐫𝐢𝐬𝐭𝐢𝐧𝐚 𝐌𝐰𝐚𝐤𝐚𝐧𝐠𝐚𝐥𝐞, 𝐃𝐀𝐑 𝐄𝐒 𝐒𝐀𝐋𝐀𝐀𝐌)
MKURUGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, amesema katika maisha yake na kile anachoishauri jamii anamaanisha na kukiishi.
Amesema kwa siku anapata
#HABARI
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Dorothy Gwajima amesema baada ya kuchanja chanjo ya UVIKO-19, mume wake ametesti 'mitambo' kwake na kukuta yupo 'fiti'./
#HABARI
MBUNGE wa Viti Maalum (CHADEMA), Easther Bulaya, ameliamsha upya Bungeni sakata la kikokotoo cha mafao ya wastaafu, akisema wafanyakazi bado wanalia na wanafanya kazi kwa kinyongo, kwa kuwa asilimia 33 inayotumika si haki yao./
#MICHEZO
UONGOZI wa klabu ya Yanga umesema upo makini katika mchakato wa kusaka kocha Mkuu na wameweka malengo ya kumpata kocha mwenye uwezo mkubwa na aliyefanikiwa kupata mataji Afrika. /
#HABARI
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imekataa pingamizi la Mbunge wa zamani wa viti Maalum (CCM), Vicky Kamata la kupinga mtoto wa ‘mumewe’, asiteuliwe kuwa msimamizi mirathi na mali za marehemu, Dk.Servacius Likwelile zenye thamani ya zaidi ya sh.bilioni
#HABARI
ZAIDI ya askari 10 baadhi yao wakiwa na silaha za moto wamedaiwa kuzingira ofisi za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (
@ChademaTz
) Kanda ya Mbeya, katika kikao cha ndani cha viongozi wa Baraza la Wanawake wa chama hicho (
@BawachaTaifa
).
Ni Kaka, Ni Godfather wa HIP HOP Bongo, Ni Mwanasiasa pia aliwahi kuwa Mbunge wa Mikumi CHADEMA,
@ProfessorJayTz
anahitaji msaada wako wa matibabu kupitia..
MPESA: 0757919192 Joseph Haule,
TiGOPesa: 0715919192 Joseph Haule,
CRDB account no: 0112044845200 Joseph Leonard Haule.
#HABARI
JESHI la Kujenga Taifa (JKT), limesema litawachukulia hatua kali za kisheria yeyote atakayebainika kueneza taarifa za uzushi kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya Jeshi hilo kwamba kuna unyanyasaji wa kijinsia kwa vijana wanaohuhudhuria mafunzo ya.../
#HABARI
MFANYABIASHARA maarufu nchini Tanzania, Rostam Azizi, na Mbunge wa Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo, wamemshukia vikali Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kwa kutoa kauli za ubaguzi dhidi ya wazanzibari kwenye mjadala unaoendelea wa uwekezaji..../
#HABARI
SAKATA la Wakili Baraka Mukama anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuzuia wateja wake kukamatwa, limechukua sura mpya baada ya mambo mengine kuibuka, ikiwamo namba ya uwakili anayodai yake, kusoma jina lingine./
SWALI: Ulionekana kwenye jukwaa la CHADEMA hivi karibuni. Je, ni maandalizi ya kurejea katika siasa?
DK. SLAA: Ninashukuru umeuliza hili. Kwanza kabisa, mtambue ya kwamba Karatu ni nyumbani kwangu na mimi ni mzee sawa na wazee wa Karatu.
#HABARI
JAJI mstaafu John Mgeta amesema changamoto iliyomuumiza katika kutekeleza majukumu yake ni kitendo cha aliyekuwa Waziri Mkuu, kudharau uamuzi wa mahakama kwa kuchana uamuzi aliotoa katika kesi ya mgogoro wa ardhi./
#NipasheJumapili
FAHAMU mgomo mwingine unaomnyemelea Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Amos Makalla, baada ya ule wa Dar es Salaam uliowahusisha wafanyabiashara wa Kariakoo kuhusu kero mbalimbali walizokuwa wakikumbana nazo. /
"Mimi ni mfungwa wa kisiasa na 302, mimi nilijiandaa kufungwa na si kupigwa faini, nilikuwa sawasawa na sitapigia mtu yeyote magoti kwa kitisho cha gereza au kuniua kwa sababu yale ninayoyapigania, ninayaamini"-Mbunge Tarime Vijijini
@HecheJohn
#HABARI
BAADA ya wanyama kupewa majina ya watu maarufu kutoka nje ya nchi, Shirika la Hifadhi za Taifa za Tanzania (Tanapa) limeanzisha utaratibu maalumu wa kuwezesha watu wanaotaka baadhi ya wanyama waitwe majina yao kufanya hivyo lakini kwa kulipia Shilingi milioni tano.
𝐌𝐀𝐙𝐔𝐍𝐆𝐔𝐌𝐙𝐎 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌𝐔
ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania Sweden, Dk. Wilbroad Slaa, Katika suala la mikutano ya hadhara, Magufuli alidanganywa na mawaziri wake waliomweleza kuwa uchaguzi huko Marekani ukiisha, siasa zinaendelea bungeni na nilikwenda nikawahoji...
#HABARI
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam,Albert Chalamila, amesema kampuni za maegesho barabarani zimeajiri vijana wasio waaminifu ambao wananyanyasa wananchi./
(𝐈𝐦𝐞𝐚𝐧𝐝𝐢𝐤𝐰𝐚 𝐍𝐚 𝐌𝐰𝐚𝐧𝐝𝐢𝐬𝐡𝐢 𝐖𝐞𝐭𝐮, 𝐃𝐀𝐑 𝐄𝐒 𝐒𝐀𝐋𝐀𝐀𝐌)
MWANAFUNZI wa udaktari, Ahlam Azam Mohamed, ameweka rekodi ya kuwa mwanafunzi mdogo kuliko wote kuwahi kutokea nchini kuhitimu Shahada ya Udaktari wa binadamu akiwa na miaka
#BREAKINGNEWS
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, ameagiza makontena 20 ya samani yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, yapigwe mnada, na kwamba hajali vitisho vya mwanasiasa huyo na ameapa kusimamia sheria na kanuni za kodi zikizopo
#NUKUU
"Mahakama Kuu imetoa hukumu kuwa Rais wa Tanzania anaweza kushtakiwa kwa makosa ya uvunjaji wa Katiba.Jaji Lameck Mlacha ametoa hukumu hiyo katika hukumu ndogo kwenye shauri nililofungua kumshtaki Rais
@MagufuliJP
kwa kumvua uCAG Prof. Assad."-
@zittokabwe
#HABARI
KAMISHNA wa Polisi Zanzibar, Hamad Khamisi Hamad, amesema wanamchunguza askari wao anayetuhumiwa kwa ushoga na ikithibitika, atafukuzwa kazi na kushtakiwa mahakamani./