SAD NEWS. Viongozi wa DARUSO wote wametimuliwa isipokuwa Makamu wa Rais. Wameambiwa mwisho saa 6 wasionekane chuoni. Kwahio Hawa viongozi walioamua kusimama kwa niaba ya wenzao, haya ndo malipo yao?
#IstandWithDarusoLeaders
#IstandWithDarusoLeaders
Kwa leo tuamke na hii zawadi ya Taifa.
PlayStation 4 Pro.
Tangu tumeanza mahusiano nilijua jinsi gani anapenda sana kucheza Game. Nami nilitamani sana siku moja nimletee zawadi, kama sehemu ya kuungana nae kwenye hiki anachokipenda.
Pia aendelee kukaa ndani wikendi 😂😂😂😂
Hatimaye jana nilitunukiwa shahada yangu ya kwanza ya Masomo ya Biashara.
(Bachelor of commerce in Banking and Financial services), Chuo kikuu cha Dar es salaam. Asante sana Mungu kwa Baraka zako.
Niliamini mimi ninastahili mume mwenye hofu ya Mungu ili pia maisha yangu yawe yenye kumkumbuka Mungu na kumuogopa. Ukibahatika kupata mwenza mwenye hofu ya Mungu hawezi kukusumbua. Atajua mipaka na majukumu yake kwako.
I Love You
@Kimkayndo
.
#ramadhankareem
#ijumaamubarak
Asante sana Mungu kwa kunipa nafasi ya kupata mwaka mpya katika maisha yangu. Sio kwa nguvu wala juhudi zangu. Haya ni mapenzi yako wewe Mungu wangu.
Hakika naona Neema zako katika maisha yangu.
HAPPY BIRTHDAY TO ME.
“Ewe Muislam mwenzangu hizi siku chache za Ramadhan zilizobaki sio za kulala kabisa, zinaweza kuwa sababu ya kubadili mfumo na mwenendo wa Maisha yako. Najua kuna uchovu pia ule utamu wa usingizi, ila vishinde vyote na uamke kufanya ibada maana Raha ya pepo ni ya milele.
Natumai surprise yangu ya Ps 5 umeipenda Sweetie wangu.
Finally nimefanikiwa kukupatia PLAYSTATION5,ulikuwa unasubiri bei ishuke ndo ununue.
Mie Uvumilivu ulinishinda nkaona wacha nilipize tukio la Anniversary ngoma iwe droo
I love You Sweetie
@Kimkayndo
Vibe la mashemeji 🙌🏻
Ukiwa unaweka “serious content” mitandaoni ni ngumu kupata followers wengi lakini ni rahisi kupata watakaokuamini na kusimama na wewe
Wanaamini katika unachokifanya utawafikia tu na wanaweza wasi-like. Tuzingatie zaidi “reach” na sio “likes” -
@miss_mshangama
#WomenAtWebTZFGD
Hii video ina historia ya kweli. Inaeleza juu ya suala la Ukatili kwa wanawake hasa kuhusu suala la kumiliki Mali na suala la VVU. Tafadhali Itazame kisha sema neno lolote.
#SemaInatosha
|
#ChukuaHatua
@OxfamTz
@Oxfam
Ni neema za Mungu zimetufikisha kuona mwaka wa ndoa yetu (14/7). Naomba tuendelee kupendana, kusikilizana na kuheshimiana. Nashukuru kwa kuwa mume bora katika maisha yangu.
Nashukuru kwa kunihamasisha kufanya ibada na kufanya kazi kwa bidii. Nakupenda sana mume wangu
@Kimkayndo
Naomba kujua kama Tz huu mzigo wa PS 5 umeshaingia.Anniversary yetu inakaribia, nifanye yangu mie. Maana hapa tangu jana story ni PS 5. Anaitaja mno inabidi tu nimnunulie. Naomba kujua pia Kulipa kwa kuchanja na Tembo Card au nitume kwa Simbanking ya
@CRDBBankPlc
#PopoteInatiki
Leo 8/6/2021 nimehudhuria Mkutano wa wanawake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.
@SuluhuSamia
. Mkutano uliobeba mada inayosema “Mwanamke na Maendeleo”. TUJITAMBUE, TUJIZATITI, TUTEKELEZE WAJIBU WETU.
Jumamosi ya tarehe 25/09/2021 nilialikwa kuwa Mgeni rasmi katika mahafali ya 18 ya kidato cha nne shule ya sekondari St. Mark’s
Iliyopo Mbagala Dar es salaam na kupokelewa na wenyeji wangu ambao ni Mkurugenzi pamoja na Mkuu wa shule kisha kuvalishwa shada na wanafunzi
Utasikia mtu anaweka sifa kibao kwa mke/mume amtakaye. Mara oooh “Nataka mume anayefanya ibada”. “Nataka nioe mke anayeswali swala tano”. My friend!! Mambo sio rahisi hivyo. Kama wewe unataka kupata mke/mume mwenye hofu ya Mungu, anza kujipiga msasa wewe kwanza.
Hamna jambo linaumiza kama tumbo la period jamani, japo natambua sio kwa wanawake wote. Ila mimi binafsi huwa nakosa amani kabisa. Yani zile tarehe zikifika huwa mambo hayakai. Maana ninaumwa tumbo balaa. Nakuwa mnyonge Kwakweli 😭😭
There is always Next Time. Hata hivyo Congo bado tuna nafasi ya Kushinda. Tunaomba tu Viongozi wa Simba watoe utaratibu wa kwenda Congo kushangilia.
#thisissimba
#HiiSijanuna
Ishu si kama watuoni au hatupendi kusapoti juhudi zinazoitwa za maendeleo. Hoja ya msingi ni kwamba, USALAMA, UHAI na UHURU WA RAIA ni muhimu zaidi kuliko SGR, Bombadia, kuongeza vituo vya Afya, Elimu Bure, Vyeti feki, na kwenda kufungua matawi ya mabenki mapya.
#ChangeTanzania
Nachukua nafasi hii kumshukuru
Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia kuwa mmoja wa walioteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa (Viti Vitatu - Bara).
Pia, naishukuru sana Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kuniamini na kuniteua kugombea.
Kwakweli mnisamehe tu. Hii ndo ilikuwa siku ya harusi yangu. Jeuri ya kupost hizi pics ni kutokana na kutumia
#MtandaoSupa
wa
@VodacomTanzania
. Harusi ni siku muhimu wacha nipost, hadi nichoke. Maana mtandao uko spidi balaa halafu kwa bei rahisi tu
Jana ilikuwa Birthday ya Sweetie wangu
@Kimkayndo
. Hakika ilikuwa siku ya furaha kwangu na kwake.
Nakuombea kheri Mume wangu katika mwaka wako huu mpya, utimize yote mema yaliyo kwenye matamanio na mipango yako. I love You ❤️
Nashukuru uongozi wa Serikali yawanafunzi wa chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM kwa kunialika kuwa mgeni rasmi. Leo katika Matembezi ya amani kupinga dhana potofu kwa wanafunzi wa vyuo. Kundi letu lilikuwa pamoja na washiriki wa mashindano ya urembo Miss IFM
#KataaMitazamoHasiVyuoni
Jana tumeungana na tumejua
@TitoMagoti
ulipo, Mungu akupe ulinzi na Afya njema. Insha Allah tumuombee na
@TheoGiyan
naye Allah amtunze na tujue yuko wapi.
#BringBackTheo
Hakuna kitu kizuri kinacholeta Furaha kama kufanya kazi unayoipenda. Unaweza usipate kipato kikubwa lakini kuishi ndoto na matamanio yako ni zaidi ya kipato.
Hata kwenye Mahusiano. Hakuna kitu kizuri kama kuwa na Mpenzi wa ndoto zako. Mahusiano ni Furaha mengine ni matokeo tu!!
Hakika vita umeipigana vilivyo. Sisi ndugu na mashabiki zako tupo nyuma yako. Haijalishi tutatukanwa na kudhalilishwa kwa kiasi gani,
@diamondplatnumz
kupitia tuzo hii nimeona ni kiasi gani watanzania tuna umoja, upendo na kuthamini vya kwetu. Tunatambua kazi kubwa uliyofanya.
Vjosa Osmani Mwanasheria amekuwa Rais wa pili Mwanamke nchini Kosovo baada ya Atifete Jahjaga ambaye amekuwa Rais kuanzia mwaka 2011-2016.
Ni Rais mwenye umri mdogo zaidi (38).
Mnamo tarehe February 3, 2020, Vjosa Osmani alichaguliwa na kuwa Spika wa Bunge Mwanamke wa kwanza.
Joanitha Kabula Mwanamke mwenye umri wa miaka 32, ambaye ni Rubani wa ndege kwenye Shirika la
@AirTanzania
Dream liner. Kwenye familia yake yeye ni wa tatu. Wakwanza ni baba ake, wapili ni kaka ake mkubwa na yeye. Ameanza akiwa na miaka 23.
#Girlpowerconference2020
Nimekuwa Mshindi wa Tatu katika shindano
@GivingTuesdayTZ
stori yangu ni,Nikiwa Makamu wa raisi wa serikali ya wanafunzi UDSM 2016 nilijitolea kuchangisha fedha za ada za wanafunzi 6 wa mwaka wa kwanza waliokuwa wamekosa mkopo na kutaka kurudi nyumbani
#UtoajiWanguHazinaYangu
Mamlaka zinajuaje labda Viongozi hawa walitumia njia ya Bandiko kwa lengo la kutuliza maandamano?? Wanafunzi wamekaa miezi miwili bila pesa zao, leo viongozi wanadai wanasimamishwa masomo badala ya kupewa maneno ya kuwafariji na kuwaelekeza walipokosea.
#IstandWithDarusoLeaders
Baada ya Harusi yangu kuisha sasa ni kupost tu pics. Na zile natumia
#MtandaoSupa
wa
@VodacomTanzania
wanazengo naomba tu mnisamehe. Maana hii spidi ya Mtandao pia inachangia hizi vurugu za kupost
Usiogope kukutana na watu wenye chuki na wewe katika safari ya mafanikio yako, hio ni ishara kuwa upo katika nafasi nzuri ya kufikia mafanikio, una uwezo zaidi yao, una maisha mazuri zaidi yao, hawajipendi na wanatamani kuwa kama wewe lakini wameshindwa Sababu wao hawana malengo.
Kuna jamaa mmoja alimpa kazi ndugu yangu hizi za mitandaoni na kagoma kumlipa.
Nakaribia kumtaja, maana haiwezekani mitandaoni mnajiweka na high profile kumbe mnafanya dhuluma ground.
Asanteni sana WAJUMBE WA BARAZA KUU UVCCM TAIFA kwa kwa kunipa kura za kishindo na kunifanya niwe MJUMBE WA MKUTANO MKUU CCM TAIFA NA BARAZA KUU UVCCM 2022-2027.
Lakini niwashukuru wale wote ambao mlinipa support kwa njia mbalimbali kuhakikisha hili linatimia ASANTENI SANA.
Binafsi taarifa za msiba wa Shammy zimeniumiza mno. Sikutegemea kupata taarifa ile japo nilifahamu anaumwa kwa muda kidogo.
Mimi sijapoteza Rafiki wa Karibu tu kama wengi wanavyofikiri. Mimi nimepoteza Dada, Mlezi, mshauri na mpambanaji mwenzangu.
Innalillah wainnaillah raajuin
Tumetembelea Makao Makuu ya Bank ya Dunia (World Bank) na kujifunza kazi na mambo mbalimbali. Na kikubwa ni kuangalia Miradi na Programu zenye lengo la kuwasaidia vijana pamoja na kupata taarifa za fursa za vijana.
#iyla2019
@IYLAinfo
@GPWTanzania
Happy Birthday Sweetie
@Kimkayndo
❤️❤️
Namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunikutanisha na wewe. Nashukuru sana kwa sapoti unayonipa siku zote.
I Love You Sweetie ❤️
Nchini Kenya Katika Sherehe za kumaliza Mafunzo ya PYPA
(Ni program ya mwaka mzima inayochukua wawakilishi vijana kutoka vyama vya Siasa
Nilichaguliwa kuwa Msichana niliyeongoza kwa utanashati (smartest lady).
katika kipindi chote cha mwaka wa mafunzo.
Watu maarufu na waliofanikiwa nadhani wanapaswa kukumbuka jamii.
Huyu Dada
@FlavianaMatata
Kwa kuanzia Lavy Pads wamewapa wanafunzi 100 pads za mwaka mzima kutoka sehemu mbalimbali.
#SikuZaoNiSikuZetu
Hii Siku ilikuwa siku mbaya sana kwa Sweetie wangu
@Kimkayndo
, pia Presha na ubize wa kuhakikisha msanii mpya
@dvoice_ginni
anaenda mjini vilimzonga. Hakulala siku tatu.
Basi ilibidi nitumie nguvu na akili kubwa sana kurudisha furaha yake katika siku yake muhimu ya kuzaliwa.
Shamira ni Mwenye Maono, Dira na Malengo ya kuleta Fursa Sawa kwa Vijana katika Kila Nyanja ya Uzalishaji wenye tija kwa Vijana wote.
Ndugu Mjumbe naomba Kura Yako ya ndio nikawe Mbaraza UVCCM TAIFA VITI 3 - BARA.
#KURA
YAKO HAIJAPOTEA CHAGUA SHAMIRA
@shamiramshangama
Unawezaje kumkamata mwanamama mwenye mimba na kumuweka mahabusu kwa kosa analotuhumiwa mume wake?
Mamlaka husika ziangalie suala hili na hatua za kisheria zifuatwe haraka iwezekanavyo.
Kama hatua hazitachukuliwa sasa, tujiandae kuona Polisi wakifanya matukio ya kinyama zaidi.
Marekani wamenionesha kwa vitendo Maana ya “Uhuru wa kujieleza”. Hakika huu ni mfano wa kuigwa sana kwa Mataifa yote Duniani hasa kwa nchi za Afrika. Eneo mbele ya White House (ikulu),Free Speech Zone. Hapa ndipo watu mbalimbali wenye lolote la kutoa kumpelekea Raisi
@IYLAinfo
Kuna wale watu wanakosea kisha wanakimbilia kusema “Ndo Nilivyo”. Hivi kama watu wote tungeachwa tuishi vile tutakavyo hii dunia ingekuwaje? Ni kweli tunatofautiana tabia, lakini kuna zile standard za kibinadamu tunazopaswa kuziishi wote. Ndio maana kuna Polisi na mahakama.
Utaifa haimaanishi kuwa Mtumwa wa fikra, si kuongea yanayowafurahisha wachache na kuwaumiza wengi, si kusifia tu bila kukemea au kukosoa. Utaifa ni pamoja na kuheshimu, kusimamia na kufuata katiba na taratibu za nchi, kulinda haki za Binadamu na mali zao.
#changeTanzania
Huu Muswada umeshapita bungeni sasa unapelekwa kwa Rais kuusaini na kuupitisha. Mh. Raisi
@MagufuliJP
macho ya watanzania yapo kwako. Ni muswada uliokiuka haki za vyama na maendeleo ya demokrasia ya nchi yetu pendwa. Tunaamini utatutendea haki kwenye hili. Asante sana
Nipo Lusaka Zambia kuhudhuria mafunzo ya siku nne ya vijana wawakilishi wa nchi za Afrika, mafunzo yanahusu jinsi ya kukusanya data kwa makundi mbalimbali ya kijamii juu vipaumbele vya vijana katika Maendeleo ya nchi.
Huu ni muendelezo wa mchakato tuliouanza mwaka 2019
Ujana ndio muda sahihi kujitolea kuhakikisha unagusa na kuinua maisha ya wenye uhitaji. Hii ni Story yangu fupi ya kuchangisha ada kwa wanafunzi wenzangu ambao walikosa ada na kutaka kukatisha masomo yao.
#GivingTuesday
#givingtuesdaytz
@GivingTuesdayTZ
Hivi wanazengo nanyi mlikuwa mnajua kuwa “Ukisema Parliament unamaanisha Rais yuko Mlee,waziri mkuu yuko mleee.. na kila mtu yuko mleeee”. Ila hapo mwisho mmesikia kuwa “JAMAA SHUJAA SANA YULE”.. huu mkono unaomlisha huyo jamaa hauogopi sijui ndo upi? Nisaidieni
#ChangeTanzania
Jana nilikuwa Jijini Dodoma katika kikao na taasisi za vijana kuunda timu ya Tanzania itakayosimamia mchakato mzima wa(African charter on Democracy, Election and Government)ACDEG.Ambapo wajumbe wa mkutano walinipa Nafasi ya kuwa mwenyekiti wa timu Tanzania.
#ACDEGTZ
@ROAAfrica
Magavana wa kikoloni walikuwa wanalindwa kwa sababu tulikuwa hatuwataki..Lakini leo hii kiongozi umechaguliwa na wananchi na wamekupigia kura kwa kukupenda lakini unakuwa na walinzi wakukulinda,wanakulinda dhidi ya nani..?"- Wakili Sungusia
#KatibaMpya
#KatibaNiYetu
Kwa Wasichana / wanawake wenzangu.
Mustakabali wa Ndoto zetu ziko kwenye mikono yetu. Kufanikiwa au kutokufanikiwa ni maamuzi yetu. Natambua changamoto bado ni nyingi sana hasa zile za kijamii na kitamaduni lakini hii isiwe sababu ya kukata tamaa na kuamini tumeshindwa
Kesho Insha Allah tunatimiza miaka minne ya ndoa yetu yenye furaha na mapenzi.
Nakupenda sana Sweetie wangu
@kimkayndo
Comment Neno lolote la kheri kwetu
Usimdharau mtu, maana hakuna ajuae kesho ya yoyote. Unaweza kumdharau leo na kesho Mungu akampandisha.
Unamkuta sehemu ambayo yeye ndo tegemeo lako kwa muda huo.
🙏🙏🙏🙏
Ni furaha iliyoje pale mgombea uliyemuunga mkono na kushiriki kuomba wengine wamuunge mkono anapoibuka na ushindi.
Hongera sana my brother January Makamba.
@JMakamba
Tumeshafika Seoul Korea kuhudhuria
Mkutano wa Amani duniani utafanyika kuanzia kesho 26 Feb kujadili juu ya Sera mbalimbali za Amani, jinsi sheria za uvunjaji amani zinavyopaswa kuboreshwa na mbinu za watu wadumishe amani
#KoreanDream
#OneKorea
#GlobalPeace
#코리안드림
Kama una uwezo wa kuongea vizuri mbele ya watu, inaweza kukusaidia kupata kazi, cheo, kutoa elimu kwa marafiki/ wafanyakazi wenzako/ jamii. Na kadiri unavyozidi kuongea mbele ya watu mara kwa mara ndivyo uwezo wako unavyokuwa mkubwa zaidi, na kujiamini kunaongezeka zaidi.
Nilishazoea kwenda shule na vyuo mbalimbali kuongea na wasichana kuhusiana na suala zima la Uongozi. Ila sasa hakuna shule wala Chuo, watu tunaogopa . Ila Sina hofu sana najua
#TemboAtaongea
Asante sana Mungu kwa kunipa nafasi ya kuuanza mwaka mpya katika maisha yangu. Sio kwa nguvu wala juhudi zangu. Haya ni mapenzi yako wewe Mungu wangu.
Hakika naona Neema zako katika maisha yangu.
HAPPY BIRTHDAY TO ME.
Mh. Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe
@jokateM
ametangaza kuwa Harambee kwa ajili ya Kampeni ya Tokomeza Ziro ya Wilaya ya Kisarawe imeahirishwa hadi hapo itakapotangazwa tena. Na kuwashukuru watu wote waliojitokeza kusapoti kampeni hii.
#KisaraweMpya
#MVNyerere
Umakini wa mtu ni pale anapofanya mazungumzo kuwa sehemu ya kujifunza. kwa kuamini kila anayezungumza nae ana jipya la kumfunza. Si lazima kila wakati ubishane au kujibu hoja zile ambazo unaziamini wewe. Pia tukubali kushauriwa japo kwa kusikiliza . Huwezi kujua kila kitu !!
Tumemaliza utafiti tuliofanya na Taasisi ya
@ShahidiWaMaji
. Utafiti ulikuwa na lengo la kufahamu changamoto na kero wanazokutana nazo wananchi katika masuala ya Maji, Usafi wa Mazingira na Mafuriko.
Kata tulizofanya utafiti ni tatu Dar es Salaam; Chamazi, Vingunguti na Kigogo.
Mtu wa Make Up hajafika mpaka sasa, na huyo ndo alipaswa kukufunga kichwani. Tulitaka akufunge mitandio inayoleta Rangi za Bendera ya Taifa. Vile huwa sikubali kushindwa nkasema naomba mnipe hio Make Up na Hiyo mitandio nijaribu kufunga mwenyewe.” Matokeo yake!! Vipi nimepatia??
Nimebahatika kuwa PYPA( program for young politicians in Africa ). Inayofundisha Uongozi, Demokrasia, Haki za binadamu. Program ya mwaka mzima inayochukua wawakilishi vijana kutoka vyama vya Siasa vyenye wawakilishi Bungeni nchi za Afrika. Hii ni ya nchi tatu za Afrika mashariki
Maono, Dira na Malengo ya kuleta Fursa Sawa kwa Vijana katika Kila Nyanja ya Uzalishaji wenye tija kwa Vijana wote. Ndugu Mjumbe Naomba Kura Yako ya ndio Nikawe Mbaraza UVCCM TAIFA VITI 3 - BARA.
#KURA
YAKO HAIJAPOTEA CHAGUA SHAMIRA
Leo nilikuwa shule ya secondary ya wasichana ya Christina iliyopo mkoani Tanga kufanya uwezeshaji na hamasa kwaajili ya kumsaidia mtoto wa kike kujiamini na kuchukua nafasi za uongozi katika jamii.
Mwanamke ni chachu ya maendeleo
@MwanamkeUongozi
Happy Birthday My Wonderful, amazing, unique, incomparable, handsome, strong, incredible Husband
@Kimkayndo
Allah atupe Umri mrefu pamoja ❤️❤️❤️. I Love You
kuna watanzania wenzetu zaidi ya 15,000 kutoka kaya 4025 hawana makaz,wamepoteza kila kitu kutokana na mafuriko.
Namba za kuchangia ni 0752820316
Jina Mwanamke na Uongozi.
Kwa mahitaji mengine wasilisha katika ofisi za Mwanamke na Uongozi zilizopo Kivulini karibu na Mlimani City
Martha
@MarthaNghambi
amekuwa Mwanamke mchapakazi juu ya masuala ya AMANI. Amekuwa daraja la mafanikio kwa Wasichana wengi sana kufikia malengo yao. Mimi ni mnufaikaji wa hilo.
Leo atazungumza hapa Uganda kama moja ya watu walioonesha juhudi katika kudumisha Amani|
#GPLCUg2018
“Sio vizuri kuwa na maadui lakini wakati mwingine pia sio vizuri sana na haiwezekani kumfurahisha kila mtu na kumfanya kuwa rafiki”.
@BintiSalha
@officielsalome
❤️❤️
Hongera sana
@FlavianaMatata
kwa kuwekeza kwenye jamii.
Asilimia 10 ya faida ya mauzo ya pedi zake inaenda kusaidia wanafunzi mashuleni kupata pads
#SikuZaoNiSikuZetu