Alhamdulillah nilifika London Jana na nipo hapa kwa mualiko kutoka Chuo kikuu cha Soas,Idara ya Masomo ya kiafrika.
Nitawasilisha mada kuhusu "MCHANGO WA FASIHI KATIKA HIP HOP" kwenye Kongamano la Baraza la Kiswahili kesho In Shaa Allah.
Taarifa zaidi zitawajia.
Ijumaa yenye Baraka sana kukutana na Professor Assad katika sala ya Jumaa pale Masjid Imam Jabir Bin Zaid , alikuwa anamaliza kusali sunnah nikamsubiri nikajitambulisha akauliza, unapiga Hip Hop ya ipi? Yenye Ujumbe mwingi au ya siku hizi? nikamwambia Napiga Yenye Ujumbe mwingi
Taifa Stars bila hamasa
Taifa Stars isiyo ya Wachambuzi
Taifa Stars iliyotelekezwa
Taifa Stars ya Hip Hop
Taifa Stars isiyoenda na Vikosi vya Wajuaji
Taifa Stars isiyo haidiwa hela
Taifa Stars iliyopangwa na kuchaguliwa na kocha.
Huwa inaenda vizuri kabisa.
TAARIFA RASMI KWA UMMA.
Namshukuru Mwenyezi Mungu nimefika salama nchini Marekani,Safari ilianza Ijumaa kutoka Dar mpaka Nairobi kisha Hadi New York na Baadaye kuelekea katika mji wa North Carolina (Carborro) katika Chuo Kikuu cha North Carolina.
Taarifa zaidi zitakuja.
Unamfahamu Professor Nguli wa Fasihi,aliyeandika Vitabu vya,Mfalme Juha,Aliyeonja Pepo na Siri?
Ni Mzee Farouk Topan,nina bahati ya kukutana naye mara kwa mara katika makongamano ya nchi mbalimbali.
Nachota sana Ufundi.
Nipo nje ya Uwanja wa
@spursofficial
Mkianza jeuri, picha ya pili nimekamatia ile kitu ya kukera bila Kupepesa macho nawajulisha mpaka Tottenham Hotspurs kilichotokea.Kwa ufupi tu ndugu yangu, kwenye masuala ya Yanga usitegemee nikatumia Akili zangu nazoandikia mashairi.🤣
Alhamdulillah.
Nimefika salama hapa Zurich,nchini Uswissi.
Nimepata mualiko wa kutumbuiza katika
@sunntigzhypher
ama Sunday Cypher.
Nitaamsha hapo siku ya Jumapili na kuendelea kuiwakilisha Bendera ya Wanangu wote wanaonikubali mpaka wale wanaosema natumia filter 😃.
Zetu Dua.
Jana tulipata wasaa mzuri sana kumtembelea Mjomba
@professorjaytz
nyumbani kwake na kubadilishana maarifa na soga mbalimbali, hakika ilikua siku nzuri sana, tumekubaliana tutayarish EP ambayo mauzo yake pesa yote itaenda katika mfuko wa Professor Jay Foundation.
Siku ya jana nilipata mualiko kutoka Chuo kikuu cha Humboldt kupitia Baraza la Kiswahili la Berlin ( BALAKI-BE) na kupewa nafasi ya Kuwasilisha mada, Wasilisho langu lilihusu, (Nafasi Ya Hip Hop katika kukuza Maadili mema 🇹🇿).
Kwa taarifa zaidi tembea IG yangu.
Mapema leo hii katika Makaburi ya Mwinyi mkuu Magomeni na Ndugu yangu katika Imani Suma Lee,tukimsindikiza Ustadh Adam Ahmad Abdallah katika safari yake ya mwisho hapa Duniani
Zimebaki siku 8 Album yangu mpya itoke rasmi.
Kama unaona huwezi kununua Album kwa njia zetu unaachana nazo unatafuta Album zingine zilizowekwa katika njia zinazokufurahisha.
Kuliko kuongea UKHANITHI na kujiona mna hoja kumbe ninyi ni Mwandiga FC na mpo nyuma kwa bao moja.
Natoa pongezi za dhati kabisa kwa Simba Sc kwa kutufunga na kudhihirisha kwamba wao ni Bora dhidi yetu.
Hakuna mchawi katika ukweli.
Simba kwa msimu huu ni bora.
Juzi tu hapa Taifa Stars walizawadiwa Milioni 500 acha hela zinazoitwa Goli la mama kwenda kwa Simba na Yanga, leo tunaambiwa kuna Harambee ya kuchangia Taifa Stars.
Innallilahi Wainnailaihi Rajiun.
Arsenal Tanzania 🇹🇿 ileee!
Kwanza kabisa namshukuru Mwenyezi Mungu kwa Mchezo kuisha Salama pili Mama yangu,Arafa Nashir Adnan pale Masasi Chigugu hakika bila wewe nisingefika hapa London.
Dakika kadhaa zilizopita nilikuwa na Professor Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili Hospital ni mmoja ya watu Fresh sana, Amenimegea madini mengi nimeshiba vya kutosha, Alhamdulillah maarifa yanaongezeka.
Sasa katika Daladala nililopanda kuna mchuano mkali sana,Dereva na Konda wake wanagonga ngoma zangu na za
@dizastavina
, Imetoka Naandika wametandika Kanisa,Kisha VVU wakaachia No Body is Safe.🙌🏿🙌🏿🙌🏿🙌🏿😃😃😃😃 Mpaka tufike Kariakoo kazi ipo.
Leo nimepata nafasi nyingine ya kuzungumza na Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Humboldt, Berlin ambao wanasomea taaluma ya Kiswahili Sanifu.
Niliwaeleza umuhimu na uzuri wa lugha ya Kiswahili na wao kutembelea Tanzania mara kwa mara wanapopata nafasi.
🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿.
Tunapinga mauwaji ya watu weusi wenzetu ambao ni wageni katika nchi ya Afrika ya Kusini.
Hip Hop haikubaliani na vitendo viovu vinavyofanywa na wananchi wasiotambua thamani ya uhai na heshima ya utu kwa mtu mweusi mwenzie.
#saynotoxenophobia
Nikiwakilisha mabingwa na wacheza Finali ya kombe la shirikisho barani Afrika
@Yanga1935
kutokea nchini Ujerumani.
Nasikitika kuzikosa mechi zote zilizosalia za timu yangu.
Dah!
Taarifa.
Namtambulisha kwenu Professor Aldin Muthembei, Mhadhiri Mwandamizi na Mbobezi Nguli wa Lugha ya Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam maarufu kama Mlimani, yeye ndiye aliyetoa nasaha za utangulizi kwa Kutuambia Mhadhiri ni Nani? Katika Album yangu.
#MHADHIRI
Inawezekana vipi sijui kwa mtu unayependa Hip Hop mpaka sasa huna Album ya Dizasta? Moja Kati ya washairi wa kweli nchini tuliobarikiwa kwa kizazi hiki na bei ni rafiki kabisa pia uuzaji ni rafiki kabisa. Mcheki
@dizastavina
ununue Album Hii haraka sana,bei ni rafiki mno.
TAARIFA:
Alhamdulillah,kila kitu kipo safi hapa London na wakati huu nimeshafika katika Kongamano na tayari kwa kuwasilisha mada yangu Lakini pia kutumbuiza kidogo kwa ajili ya kuendelea kuitangaza lugha yetu ya Kiswahili.
Taarifa zaidi zitawajia kupitia CBTV CHAMAZI BAMIA TV.
Jana nilipata wito kutoka kwa Dokta Husein Abass Katibu Mkuu wa Wizara ya Michezo,Sanaa na Utamaduni,Kujadili na kuona namna bora zaidi ya kuutumia ule ubeti wangu nilioupiga katika jukwaa la
@worldemcee
ambao una ubunifu wa kipekee wa kutangaza Vivutio vyetu.
Royal Tour Verse.
Mh.Rais leo amewataka Wasanii watumie nyimbo zao kuelimisha jamii, Mlio karibu na Mh. Mwambieni hizo nyimbo za aina hiyo haziuzi na ndiyo maana hata Wasanii wengi waalikwa si wenye nyimbo za aina hiyo.
Shukrani.
Hamburg ➡️ Gothenburg Sweden.
MHADHIRI SUGU
Asante Mjomba Sugu kwa kuniita na kununua Album yangu mpya ,si mara ya kwanza wala ya pili kununua kazi zangu na kila tunapokutana huachi kunipa nasaha na kunieleza furaha yako kila unapoona Harakati zangu zikienda katika njia Chanya za mafanikio.
@TheRealJongwe
Unajua mimi Hip hop yangu naifanyia Rotesheni,paap, Marekani,paap Ujerumani,paaap tena Uingereza, kwa hiyo striming ukiweka na rotesheni ni simpo kuwadaka new fans na mashabiki pia katika market strateji ya Coffee Maker.
Ivo Yani.
Hazina Sura Ya Kwanza -Mixtape 2011
Mzimu wa Shaaban Robert - Album 2012
Chizi - Mixtape 2013
Mchochezi -EP 2014
Diwani Ya Maalim - Album 2019
Tumehitimu EP - 2020
Vitasamoto - Album 2020.
+ Bonus Ya Single 15.
Zote kwa 30,000/=
Kwa Wanunuzi wa kweli njoo WhatsApp 0769522346.
Mwanangu wa Pili wa Kiume, Nashir Mutalemwa Mushumbusi leo Katika mahafali ya kuhitimu Elimu ya Awali, ametangazwa kuwa Mwanafunzi Pekee aliyefanya vizuri katika Somo la Kiswahili. Mhaya amejizaa. Shukrani kwa Mwenyezi Mungu.
TANZIA.
Dada yangu wa 3 kuzaliwa wa mama mmoja, Kulwa Ofula, amefariki jioni hii ya leo katika Hospitali ya Ndanda,Masasi.
Maziko yatafanyika kesho saa 10 alasiri Kilwa Kivinje. Insha Allah.
Mwenyezi Mungu amuweke Panapostahili.
M.A.P