Nimeambiwa kuwa Wasafi FM Leo asubuhi wamenichafua saana na kusema kuwa Mke wangu ni Mbunge kwa sababu tu nilimtaka Spika wa Bunge aache Propaganda.
Ndugu Maulid Kitenge aniombe radhi Ndani ya 24 hours as Sina mke Mbunge na sijawahi kuwa naye. Asipofanya hivyo nitajiongeza!
Usiku huu nyumba ya mgombea ubunge wa Chadema Chato imenusurika kuunguzwa na moto, nyumba ya diwani wetu wa Mganzo imevamiwa na wahalifu hao na wamevunja mlango ila wamezidiwa na nguvu ya wananchi. Wanatumia Gari mbili land cruiser wamekimbia. Kesho Rais Lissu atakuwa Chato!
Nimetangaza Nia ya kugombea Ubunge Jimbo la Segerea Katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu kama Chama changu Cha Demokrasia na Maendeleo-Chadema kitanipa fursa hiyo.Naomba ushirikiano kwa wananchi wa Jimbo hili.
Msigwa ametoka Magereza pamoja na ukweli kuwa tuliwalipia watu watatu ila aliyetolewa ni Msigwa . Msigwa amekataa kupanda magari ya serikali na kuongea na vyombo vya habari vilivyoandaliwa na Polepole ambaye Yuko segerea. Sasa Msigwa yupo na wakili wa Chadema. Tutawapa updates
Humphrey Polepole Muda huu anamtukana Mgombea Urais wa Chadema kuwa ni msukule ndio maana watu wanaenda kwenye mikutano yake ili kumshangaa! Matusi haya yanatangazwa live na TBC redio na nyinginezo .
Maadili ya uchaguzi yanavunjwa waziwazi na hakuna wa kuchukua hatua.
#SasaBasi
Pichani ni DAS wa Kisarawe Mtela Mwampamba ambaye uteuzi wake umetenguliwa Leo na Rais kwa tuhuma za kutembea na wake za watu. Aliyekaa kulia Kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwengelo.Mtela alifukuzwa uanachama wa Chadema na Bavicha kwa makosa ya utovu wa nidhamu 2013
Managment ya Clouds Media Group, inawezekana hamkuwatuma wale waandishi wenu Leo asubuhi kuitukana na kuidhalilisha Chadema kwa maneno ya uongo, Kama ndivyo semeni tujue au laa tutajua mliwaelekeza kufanya waliyofanya, tupeni sababu ya kwanini tuwasikilize. ..
@CloudsMediaLive
Mpaka saa tatu kamili usiku huu michango imefikia kiasi cha shilingi 36,547,000 na zinaendelea kupokelewa. Hizi ni nje ya zilizotumwa kwa njia ya Benki ambazo tutatolea updates asubuhi . Tunashukuru kwa mchango naomba muendelee kuchangia tafadhali.
Tuna taarifa za uhakika kutoka Vyanzo vyetu kuwa Vijana wa Green guard kutoka Arusha walioondoka kwa ajili ya kazi maalum wamefika Singida.Tunaendelea kufuatilia kwa karibu kazi hiyo waliyotumwa wataitekeleza vipi..Miongoni mwao ni wale waliofuzu 'mafunzo maalum' hivi karibuni!
Ndugu zangu maisha ni mafupi sana, dakika chache zilizopita Dereva wangu jimboni Segerea amempoteza Mama yake mzazi, amegongwa na gari alipokuwa anavuka barabara kwenye Zebra hapo Magengeni Liwiti.
Tumuombee aweze kupata uvumilivu na nguvu za kuhimili matatizo haya.
Updates kuhusu Mdude Nyagali:
Alikamatwa na Polisi juzi tarehe 10.05.2020 na alituhumiwa kwa Makosa ya uchochezi wa mtandaoni. Jana Polisi walienda kufanya upekuzi nyumbani kwake na 'dalili' zilionyesha kosa la mtandaoni sio kinachopekuliwa kwa taarifa za mashuhuda . Tumuombee!
Breaking News : Msafara wa wagombea mbalimbali wa Chadema walio enguliwa kugombea uliokua unaelekea tume ya Taifa ya Uchaguzi Dodoma umekamatwa na police Muda huu.
Wakili John Mallya anashikiliwa na Polisi Kituo kikuu cha Morogoro kwakosa la kumtishia msimamizi wa Uchaguzi Morogoro Mjini kuwa atadeal naye personally kisheria iwapo angeendelea kumnyima fomu za rufaa Devotha Minja baada ya kumuengua kihuni.Tutawapa tariff zaidi
Baada ya kauli kuwa Barakora ni sawa na titi la Mwanamke lililokatwa, nilitegemea kusikia kauli za wanaharakati na wanawake kutoa sauti kubwa. ...ila nimewasikia wachache sana wakipaza sauti...Wanawake ni jeshi kubwa mnaweza kujitetea na kukomesha kauli za aina hii. Nawapenda!
Ndugu Watanzania wenzangu, Kwanza Niombe radhi kwa kuchelewa kutoa updates ya michango na sababu Kubwa ilikuwa ni reconciliation ya Namba zote ambazo zilikuwa zinakusanya as kulitokea tatizo la kiufundi Jana na tumelitatua tayari. Nitaweka updates soon . Asanteni sana
Sasa ni rasmi mimi ni Mgombea Ubunge Jimbo la Segerea kwa Tiketi ya Chadema. Pambano limeanza rasmi na Leo nitatambulishwa rasmi viwanja vya Mbagala Zakhiem kabla ya tarehe 30.08. Kutambulishwa viwanja vya shule ya Msingi Liwiti na Mhe.Rais Tundu Lissu. Naomba ushirikiano wenu
Ndugu zangu, Jamaa na Marafiki hapa Tweeter, shughuli ya kampeni imeshaanza. Naomba mshiriki Katika kampeni zangu kwa kunichangia .Mchango huo utumwe Benki kwenda NBC akaunti Na. 011201257390.Tumia simu yako, Napokea kiasi chochote utakachotuma. Mungu akubariki, Asante Sana.
Updates 5: Makusanyo ya fedha Mpaka Leo saa nane mchana .
1. Simu 176,945,600
52,743,400
3. Cash 4,000,780
Jumla tumekusanya 234,469,000
Matumizi sh.40,000,000 Mdee, 30,000,000 Bulaya na 30,000,000 Matiko. Faini zao zimeshalipwa.
Asanteni watanzania
Tutatoa updates ya pili saa Sita usiku juu ya michango tunavyoendelea kupokea . Watanzania wameamua kuihami demokrasia kwa umoja wao. Wapo wanaochangia shillingi mia mbili, tunawashukuru sana na Kuna wanaotuma ujumbe kuwa kesho Watauza kuku au Mayai waweze kuchangia. Asanteni
Kwa wale watanzania wanaoniuliza kuhusu utaratibu wa kumdhamini Mgombea Urais Tundu Lissu. Ni kuwa uko hivi, siku anapofika Mkoani kwako utatakiwa kwenda Ukiwa na kadi ya mpiga kura ambayo imehakikiwa na ipo kwenye daftari la wapiga kura.Ukiwa umejiandikisha utapata fursa hiyo.
Uongozi ni kuwa Mfano, Pamoja na yoote angalau angeweza kutuvusha kwa kuonyesha Mfano wa kujali maelekezo ya wataalamu wa afya na WHO. ..but amerudi utumwani. ....sad .....OK amshauri Mkubwa kuzingatia ushauri wa wataalamu. ....
Historia Ina tabia ya kujirudia, waliowahi kushinda kura kwa 99.8% ni pamoja na Sadam Hussein, Muamar Ghadaf, Robert Mugabe, Hugo Chavez na Leo 2020 CCM wamevunja rekodi ya mgombea wao ametangazwa kupata 100% ya kura za Mkutano mkuu. ......Historia haijawahi kudanganya....
Ndugu Watanzania tunawashukuru Sana kwa michango yenu .Mpaka Muda huu 6:15 tumepokea jumla ya shilingi 312 Milioni. Tunatangaza rasmi kuwa tumesimamisha michango kwa zile namba nyingine zote isipokuwa namba ya Chama 0744 446969 itaendelea kupokea michango ya ujenzi wa Chama.
Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mhe.Freeman Mbowe Leo jumapili tarehe 17.05.2020 kuanzia saa saba mchana atahutubia Taifa kuhusu masuala mbalimbali nchini. Atakuwa mubashara kwenye Mitandao mbalimbali.
Kama China wameweza kuthibiti huu ugonjwa wa Corona kwa miezi miwili , na wamefanikiwa kwanini sisi Tanzania tuanze kufikiria kushindwa ? Tufikie kufikiria hata kuahirisha uchaguzi Mkuu ujao kwa hoja kuwa Bunge haliwezi kupitisha bajeti ya Uchaguzi? Tujipange kuzuia maambukizi
Kesho jumatatu tarehe 16.03.2020 saa Sita Kamili mchana, ofisi za Makao Makuu ya Chama Kinondoni Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe.Freeman Mbowe atazungumza na vyombo vya habari. Waandishi wote mnakaribishwa kufika kwa wakati. Asanteni.
TAHADHARI NA ONYO:
Mgombea Ubunge,Jimbo la Segerea wa ACT Maharagande UNAPOTOSHA Wananchi kuwa nimejitoa Kugombea Ubunge.
Najua hujafanya kampeni kwa kipindi chote,NAKUONYA UACHE UONGO HUO MARA MOJA!
WANANCHI WA SEGEREA NAOMBA MPUUZENI MUONGO HUYU,Tujipange kulinda ushindi
Ccm Karagwe wanavuruga kanuni za uchaguzi Sasa wanatumia gari la Halmashauri namba DFP 5445 kutangaza mkutano wa KAMPENI wa Kasimu Majaliwa.Tume ya Taifa ya uchaguzi iko kimya kana kwamba Maadili hayajavunjwa .
Mgombea Ubunge Karagwe ameshawasilisha malalamiko kamati ya Maadili
Updates on Michango hadi mchana huu.
1. Mapato jumla 260,084,250
2.Matumizi
Tarehe 11.03.2020 kulipia faini (3) 100 M .
Tarehe 12.03.2020 zimelipwa 100M (tunasubiri risiti ya Mahakama)
Tuna upungufu wa sh. 60M
Simu ukomo 5M kwa siku isipokuwa No.ya Chama tuliyoipata Jana mchana
Polisi wametoa hukumu,wanasema wanaendelea na uchunguzi na wanaomba wananchi wawape taarifa.Hilo hitimisho la kuwa"mlevi' si ndio mmekamilisha uchunguzi wenu?Tunajua hamjawahi kuchunguza matukio ya aina hii tangu, Ben,Azory, Lissu, Kanguye nk.Propaganda hazijawahi kushinda ukweli
Ndugai, hizi ni kanuni zinazowataka wabunge wa Chadema kukichangia Chama , na wabunge kabla ya kugombea walizisoma na kuzikubali. Kumshambulia Mbowe kuwa michango ameagiza ni UONGO.Aidha tuna taarifa za wabunge wa CCM na CUF kuchangia vyama vyao pia .
Vifaa vya kupima wagonjwa wa Corona vilivyotolewa na WHO na kukaa bandarini kwa Zaidi ya wiki 3 visambazwe kwenye hospitali zote za Mikoa na Wilaya zote za mipakani ili iwe rahisi kupima hukohuko, tusisubiri sampuli kutumwa Dar pekee. Hii itasaidia kukabiliana na maambukizi
Tutafanya mkutano na waandishi wa Habari Leo saa tano na nusu asubuhi . John Mnyika, Salum Mwalimu na Peter Msigwa watazungumza baada ya kutoka Magereza . Tutatoa updates ya michango tulipofikia
Tumeishauri Serikali kuchukua hatua nane ili kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya Corona;
1. Vifaa vilivyotolewa na WHO kwa ajili ya kupima Corona visambazwe kwenye Hospital za Mikoa zote na zile za Wilaya za Mipakani ili kurahisisha upimaji.
2. Tuzuie Wageni kuingia nchini
Ndugu watanzania tumefanikiwa kusajili Namba ya Chama kwa Jina la Chadema yenye uwezo mkubwa wa kupokea fedha nyingi nayo ni 0744 446 969 ni Vodacom. Tutaweza kutibu tatizo la fedha Kujaa kwenye simu za awali na kushindwa kutuma . ASANTENI SANA
"Vita ya Corona ni ya kisayansi nasio ya kidini, kutegemea rehema za Mungu bila kuchukua tahadhari na mikakati ya kisayansi, kibajeti, kielimu na ushirikishwaji umma ni udhaifu mkubwa wa watawala ambao utawaletea lawama huko tuendako,"Freeman Mbowe, M/Kiti CHADEMA
Mara baada ya hukumu ya viongozi wetu inayoendelea kusomwa Katika Mahakama ya Kisutu itakapokamilika, Chama kitazungumza na waandishi wa Habari Makao Makuu Kinondoni. Tunawakaribisha waandishi wote.
John Mrema .
Familia ya Freeman Mbowe yakiri kuuguliwa na mgonjwa wa Corona ambaye ni mtoto wa Freeman wa Kwanza Dudley . Familia imetoa taarifa rasmi na kuitahadharisha serikali kujidhatiti kupambana na janga Hilo badala ya Propaganda zinazofanywa.
Aliyekuwa Naibu Supika Tulia Akila chips yai kwa mama ntilie Mbeya. ..eti anawazuga wanaMbeya kuwa ni mwenzao. ...huku akiwa na security detail ya kutosha. ....Msimu wa maigizo umewadia. ....
Ili mtu ateuliwe kuwa Mbunge V.Maalum anatakiwa kujaza fomu za NEC namba 8D ambazo sehemu C Inatakiwa kujazwa na Katibu Mkuu wa Chama, na kiapo mbele ya Hakimu. NEC imepokea hizo fomu? Nani alizijaza?Nusrat alizijazia magereza?Hakimu gani alimuapisha?
Kesho Ijumaa tarehe 29.05.2020 Chama kitafanya Mkutano na waandishi wa Habari na kuzungumza na Watanzania. Tunawakaribisha waandishi, kuhusu Muda na eneo mtajulishwa hapo baadaye. Wote tuzingatie kanuni zote za kujikinga na maambukizi dhidi ya virusi vya Corona.
Huu msimu hatari sana huko Jimbo la Mbeya Mjini. ...Tulia Ackson 'apagawa' baada ya wajumbe kutokufika, aamua Kuyaruka majoka kwa staili yake. ....Vunja Mbavu. .....
Breaking News;
Tunawaalika waandishi WA Habari saa Tatu Kamili usiku huu Ijumaa 27.11.2020 katika ukumbi wa Bahari beach hotel inakofanyika Kamati Kuu ya Chama.
Mhe.Freeman Mbowe , Mwenyekiti Taifa atazungumza .
Updates 2: Tunawashukuru sana watanzania kwa umoja na michango yenu inayoendelea kupokelewa. Mpaka saa Sita usiku huu tumepokea shillingi 69,346,500 kwa njia ya mitandao na cash. Hii ni pamoja na hujuma zote ambazo tutazisema, Tuendelee kuchangia. Asanteni watanzania.
From LissuACTION ALERT!Nimetaarifiwa kwamba watu wasiojulikana wakiwa kwenye magari matatu yenye usajili T370 DRD Toyota Noah; T721 CYT Landcruiser and T132 CUP Toyota Landcruiser wananisubiri kunikamata au kuniteka nyara nje ya ofisi za Tume mara nitakapotoka nje ya jengo la NEC
Chadema Mbeya Mjini wakishiriki Msiba Leo, Wanawake hawa wamenifurahisha sana walivyoenda kumpa faraja aliyekuwa Diwani Viti Maalum Christina Sokolo kutoka kata ya Nzovwe aliyefiwa na Baba yake mzazi.
Hii picha inatuma ujumbe mzito Sana kuwa Job Ndugai yupo wapi? Anaumwa au ndio Yuko chini ya Kaunda suti ? Mbona hayupo kwenye tukio muhimu kama hili la kumkabidhi madaraka Spika Mpya?
Msimamizi wa Uchaguzi Morogoro Mjini amekamilisha uhuni wake na amebandika fomu kuwa hajamteua Devotha Minja eti hakuwasilisha picha wakati Kuna ushahidi wa video akiwasilisha kila kitu. NEC mambo haya yanaharibu Amani ya Nchi chukueni hatua haraka kunusuru Hali hii.
Mgombea Urais wa Chadema Mhe.Tundu Lissu akipokea fomu za Uteuzi wa kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa ameambatana na Mgombea Mwenza Salum Mwalim.
Mambosasa ulisema walivamia gereza, huu ushahidi unaonyesha walivutwa kuelekea geti la gereza .....watu waliostaarabika hawawezi kufanya mambo ya aibu kama haya. ....
Updates 3: On Mdude.
Tumepokea taarifa kuwa Polisi Mbeya wanamtafuta Katibu wa Kanda ya Nyassa, Ndugu Emmanuel Masonga ili wamuunganishe na Mdude . Wamekerwa na kitendo cha Masonga kusema hadharani kinachoendelea kupangwa nao kuhusu tuhuma za Mdude. Tutaendelea kueleza umma.
Walivyoumbuka Leo wakina Polepole kwa Msigwa kuwakataa hadharani na kuondoka na wakili wa Chadema. Aibu ya karne hii. ...Tumalizie michango ili Mbowe na Heche watoke Gerezani kesho. Watanzania tuonyeshe nguvu ya umma ilivyo madhubuti dhidi ya udhalimu.
TCRA, kumbe tunahitaji kibali ili kupata Namba ya kuhabarishana kuhusu misiba ? Mbona kanuni hii itamfunga kila mtu ? Tuelezwe Sasa Namba zetu ni kwa ajili ya Aina gani za Habari !
Leo sijaona picha ya kiongozi yeyote wa serikali aliyeenda kupiga kura mtaani kwake, hivi nao wamepuuza wito wa Baba Askofu Nyaisonga ? Viongozi mliokuwa mnasema Kuna uchaguzi Leo Mbona hamkushiriki ? Au nanyi mmeungana nasi kujitoa ? Tutaelewana tuu ....
Katibu Mkuu wa Chadema Muda huu anaendelea na live streaming juu ya maamuzi ya Vikao vya kamati kuu vilivyomalizika Jana usiku . Anapatikana Chademamedia, Millard na Global TV
Kama watu wanaweza kughushi nyaraka na zikawawezesha kuwa wabunge, wakatunga sheria zikiwemo za kuwa kugushi ni kosa la jinai, vyombo vya uchunguzi vipo kimya! Hivi kuna uhalifu mkubwa kuliko huu? Vyombo vya uchunguzi vinakaa kimya Kwa Maslahi ya Nani?
#KatibaMpyaNiSasa
Huyu kijana anaitwa Masumbuko Chakachua wa Kata ya Bulyankulu Leo tarehe 22Novemba,2021amenikabidhi mchele kilo 100 Kwa ajili ya kuifikishia Familia ya Mhe.Freeman Mbowe kama zawadi ya Christmas wakati huu ambao Baba Yao yupo Gerezani,Ukonga ni Upendo wa Agape huu. Ameniliza!!
Viongozi, Wanachama na wafuasi waliokamatwa na kupigwa na kuumizwa Sana na askari Magereza Leo Katika gereza la Segerea hatimaye wamepata dhamana ya Polisi na Sasa wanaelekea hospitali kwa ajili ya Matibabu. Tutaendelea kueleza hatima ya afya zao baada ya vipimo vya Madaktari
Nawapongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kusimamisha ndege zote kutoka nje ya nchi kuingia znz kama Hatua ya kuzuia maambukizi ya Corona. Wamekataa watalii, huku bara Hawaoni hiyo hatari?
Tumekamilisha kumlipia Mhe.Freeman Mbowe na Sasa ni taratibu za kumtoa Magereza zinafanyika ili atoke mchana huu Mara taratibu zitakapokamilika .Asanteni Sana watanzania
Breaking News;
Jeshi la Polisi Dodoma wamevamia ofisi za Chadema Dodoma na wanawafukuza waandishi wa Habari ambao wamezingatia masharti yote kuhusu Corona waliokuwa wanamsubiri Mhe.Freeman Mbowe, M.kiti Chadema na KUB kwa ajili ya press conference kuhusu Corona na Hali ta taifa
Masoud Kipanya na Chadema! Wakati wa Maridhiano,tukawa Mbwa na Joka , Chaguzi Kanda Malori ya mafuta yanafuata moto! Leo basi limepasuka barabarani! What next ? Au ndio utabiri hautaki kutimia!
Nikisaini fomu za maadili mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi Leo 25.08.2020 baada ya kurejesha fomu za uteuzi kugombea Ubunge Jimbo la Segerea.
Nimekamilisha taratibu zote za kuwa Mgombea Ubunge.
Msajili wa Vyama, acha kuinajisi ofisi ya umma . Huyu katengeneza mabango kabisa hujawahi kumhoji, na Kuna video Dr.Bashiru akimsifia Huyu na Cheyo ...hujasema lolote. ...mwaka huu utaisoma namba. ....
Gari la Magereza MT0128 linasambaza na kupandisha bendera za CCM Leo tarehe 07.07.2020 huko Dodoma. Huu ni uvunjaji wa sheria za Nchi na ni kinyume na mikataba ya kimataifa kuhusu haki za wafungwa. Tunalaani kwa nguvu zote tukio hili.
#Tutatumiavyombovyadola
kubaki madarakani