Dk. Shein kuhusu virusi vya corona" Si maradhi yanayotaka mzaha, si maradhi yanayotaka watu wawe wakaidi, si maradhi watu waone kweli kuna tatizo maradhi haya ni ya watu wote".
Rais wa Zanzibar na MBLM Dk. Hussein Ali Mwinyi amemtakia kila la heri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika siku yake ya kuzaliwa leo. Dk. Mwinyi amemuombea Mama Samia maisha marefu na afya njema. Happy Birthday Mama Samia
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa Mtaa wa Kwaboko mara baada ya kutoka msikitini kwa ajili ya Ibada ya sala ya Ijumaa katika Msikiti Kubba uliopo Kwaboko,Mkoa wa Mjini Magharibi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amempongeza mwekezaji mzalendo Mohamed Abdallah Mohamed, Mkurugenzi Mtendaji wa Zanzibar Cable TV kwa kujitolea kujenga jengo la kuhifadhia maiti katika hospitali ya Mnazi Mmoja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameondoka nchini leo kuelekea Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu (U.A.E) kwa ziara ya siku tatu.
Nataka kuengeza idadi ya watalii ili kukuza pato la Serikali "Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi" katika ziara yake Abudhabi
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewasili kisiwani Pemba leo kwa ziara ya kikazi ikiwa ni miongoni mwa shamrashamra za miaka 58 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesisitiza haja ya kupewa kipaumbele suala zima la usafi wa Mji wa Zanzibar kwani bado hajaridhika na hali ya usafi ilivyo hivi sasa.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi atazungumza na Wandishi wa Habari ifikapo saa 4:30 za asubuhi, Ikulu Zanzibar,.
Matangazo hayo yatarushwa moja kwa moja kupitia ZBC TV.
Rais wa Zanzibar na MBLM Mhe.. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amemtakia kila heri Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim kwa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa leo kwa kutimiza miaka 80. Mhe Dk. Hussein Mwinyi anamtakia Mwenyezi Mungu ampe afya njema mwanamapinduzi huyu wa Afrika.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Jeshi la Kujenga Taifa na Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU) na kusisitiza haja ya kuimarishwa ili mafanikio zaidi yaweze kupatikana.
Nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) wameiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupatiwa kiwanja kwa ajili ya kujenga Ubalozi mdogo ombi ambalo tumelikubali na kiwanja kipo tayari kwa ajili yao. "Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi" katika mazungumzo yake na Vyombo vya habari.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi leo ametoa sadaka ya futari Mkoa wa Mjini Magharibi katika mwendelezo wa sadaka kwa Watu wenye mahitaji maalum katika Viwanja vya Mapinduzi Square Michenzani Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, leo ametoa salamu za pongezi kwa njia ya simu kwa Mama Mariam Mwinyi pamoja na wale wote waliomuunga mkono katika uzinduzi wa Taasisi yake ya Zanzibar Maisha Bora Foundation.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewanasihi wafanyabiashara wenye tamaa kutoutumia mgogoro wa Urusi na Ukraine kuwa ni kisingizio cha kupandisha bei za bidhaa katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
"Kuna mradi unakuja wa kuhakikisha Barabara za ndani ya Mji hapa Mjini tunaziwekea Lami" Dk Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa ujio wa Rais wa Shirikisho la mchezo wa kuogelea duniani (FINA) hapa Zanzibar utasaidia kwa kiasi kikubwa kuitangaza Zanzibar kiutalii hasa katika utalii wa michezo.
Rais wa Zanzibar na MBLM Dk. Hussein Ali Mwinyi amempongeza Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza Tony Balir kwa kutekekeleza kwa vitendo ahadi zake za kuendelea kuiunga mkono Zanzibar hasa katika mipango na mikakati ya upangaji wa vipaumbele kwa watendaji wa Serikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi .Hussein Ali Mwinyi amesema hatua ya ujenzi wa hospitali 11 kwa kila Wilaya ni sehemu ya Mapinduzi makubwa ya sekta ya afya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu waliofariki kufuatia ajali ya basi lililogongana na lori huko katika eneo la Melea, Kibaoni, Mkoani Morogoro.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameeleza azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuzijenga barabara zote za Mji wa Zanzibar na kuziwekea taa, kuzipanda miti maalum pamoja na njia za wanaotembea kwa miguu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi atazungumza na Wandishi wa Habari na Wahariri wa vyombo mbali mbali Siku ya Jumatatu saa 4 za asubuhi ya tarehe 28/2/2022, Ikulu Zanzibar.
"Katika hatua tunazozipiga za kutafuta wawekezaji katika maeneo mbali mbali wenzetu wa Oman wameweka mkataba mwengine utakaopelekea wa kuwa na mji mpya wa Malindi" Rais wa Zanzibar na MBLM Dk. Hussein Ali Mwinyi alishuhudia kufungwa kwa mkataba huo, Ikulu jijini Zanzibar.