Ni haki ya beki kumkaba straika.. Ila hili la jana la wachezaji wa Kagera kumchezea rafu za makusudi Phiri halikubaliki.. Waamuzi wanapaswa kuwalinda wachezaji aina ya Phiri..
“Wewe unanifatafata sana, hii ni mara ya tatu, sikuogopi kwa lolote,kwa chochote na huwezi kunifanya chochote. Nina uwezo wa kukufanya chochote na huna cha kunifanya.” Maneno ya Hajji Manara aliyomwambia rais Karia siku ya fainali ya ASFC kule Arusha.
Huwa nasema kila siku.. Lakini leo narudia tena.. Kwenye Ligi yetu hakuna mchezaji wa kufananishwa na Chama... HAKUNA..Chama yupo mmoja tu.. Anaishi dunia ya peke yake..
Pamoja na sare ya jana.. Ukweli ni kwamba Simba msimu huu wako vizuri kuliko Yanga.. Wanapiga pasi.. Wanashambulia kwa mipango.. Na wanatumia nafasi vizuri..
Hii pesa Msuva anatakiwa kulipwa na Wydad anaweza kudhamini timu tano za Daraja la Kati kwenye Ligi Kuu... Tukiwaambia wachezaji wakacheze nje wawe wanaelewa... Bongo kuna pesa, ila nje kuna utajiri
“Yanga ina quality kubwa kuliko Al Hilal, mtu anayeweza kunichallenge aniambie wanatuzidi wapi ? Fedha na uwekezaji Yanga ndiyo nyumbani kwake,” Ally Kamwe
Rabbi Hume.. Zile picha za magoli makali ya Sakho na Phiri ni kazi ya mikono yake.. Amepewa vifaa vya kisasa.. Halafu anapiga picha za viwango vya dunia
Robo fainali Simba inaweza kukutana na Mamelodi Sundowns, Al Hilal, JS Kabylie, CR Belouizdad, Esperance de Tunis ama mabingwa watetezi Wydad Athletic Club… Unatamani Mnyama akutane na nani?
Barbara Gonzalez.. Tangu aingie Simba amesaini mikataba na M Bet, Africarrier, Emirates Aluminium, Azam TV na Vunjabei ambayo inaipatia Simba zaidi ya Shilingi Bilioni 63.. Hakika huyu dada ni Mwamba 🙌
Achana na kiwango chake cha jana.. Ninachomsifu huyu Bwana Mdogo, Ally Salim amekubali kuwa golikipa namba tatu Simba kwa mwaka wa tatu sasa.. Na bado amezidi kuwa imara.. Atafika mbali.
Yanga ikiwa na mziki kamili ilichemka hapa Ihefu.. Azam hivyo hivyo.. Ila Simba bila wachezaji SABA wa kikosi cha kwanza imeshinda.. Wanastahili pongezi.. Ila huyu Baleke ni mtu hatari sana.
Ni kweli Simba amewahi kuzifunga Al Ahly, Zamalek.. JS Soura.. na nyinginezo.. Ila alizifunga hapa Dar siyo Arabuni.. Mwaka 2003 Simba alimfunga Zamalek 1-0 Dar.. Akapoteza 1-0 Misri na kushinda kwa matuta.. Msichanganye vitu.. Yanga ameshinda 1-0 Tunisia.. Ni Historia
Kwahiyo Maafisa Habari wengine kufanya Media Tour ilikuwa sawa... Ila kwa kuwa
@AliKamwe
amefanya Media Tour wiki moja akaujaza Uwanja wa Mkapa tunaona siyo sawa.. Mbona watu tunakuwa na wivu hivyo?
Pape Sakho na Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez wameshindwa kuondoka Morocco kurejea Misri baada ya timu kadhaa kutaka kumsajili nyota huyo kwa haraka.. Wanataka kumalizana na Simba leo ama kesho. Baadhi ya Timu za Morocco na Ulaya zimeongeza nguvu kuinasa saini ya Sakho.
Yanga ndio timu ya kwanza kutoka Tanzania kupata ushindi kwenye ardhi ya Mwarabu...Nielewe vizuri.. Siyo kumtoa Mwarabu.. Bali kupata ushindi katika ardhi yake.. Kweli Yanga ni DUDE kubwa..
Mwaka 2015 aliyekuwa kocha wa Simba, Dylan Kerr alisema endapo Ajibu atajituma kwa asilimia 60 tu ya uwezo wake angeweza kucheza Ulaya.. Miaka saba baadaye Ajibu yupo Singida..
Singida Big Stars ikishinda mechi mbili zijazo za Ligi Kuu rasmi itakua imekata tiketi ya kushiriki Kombe la Shirikisho Afrika mwakani kwa mara ya kwanza katika historia