Ndege inayowasili Nchini kesho aina ya B767-300F ina uwezo wa kubeba tani
54 za mizigo na kuruka kwa masaa 10 angani bila kutua.
Ndege hii inatumia mafuta kidogo ukilinganisha na Ndege nyingine za aina hiyo.
Kuwasili kwa Ndege kutaifanya
@AirTanzania
kuwa na Ndege 12.
Mwaka 2016 tarehe na mwezi kama huu akaunti hii ilifunguliwa kwa ajili ya kutoa elimu/habari zinazohusu sekta 3 zilizo chini ya Wizara hii,tunaendelea kuwashukuru kwa maoni/ushauri ambao mnaendelea kuutoa,tunaahidi kuendelea kushirikiana nanyi kwa kuwapa taarifa mbalimbali.
Ilikuwa ndege ya kutoka wapi kwenda wapi na ilitakiwa kuondoka sa ngapi na mkaondoka sa ngapi? kwa taratibu za kawaida za usafiri wa anga kuna taasisi inaitwa TCAA-CCC panapokuwa na ucheleweshaji bila tarifa taasisi hiyo iko kwa ajili ya kuhakikisha abiria wanapata haki zao.
Ndege ya Shirika la Ndege la
@FlyRwandAir
ikipakia mizigo ya samaki kutokea Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuelekea nchini Ubelgiji ikiwa ni safari yake ya kwanza
Muonekano wa barabara ya Bwanga- Biharamulo (km 68), ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami umekamilika, barabara hiyo inaunganisha mkoa wa Kagera na Geita.
Barabara ya Igawa – Tunduma (km 218) kufanyiwa usanifu na kujengwa kwa njia nne (4), ambapo moja kati ya hizo 4 itatumika kwa ajili ya malori tu.
Mradi huo utahusisha ujenzi wa barabara ya mchepuo (ByPass) ambayo itapita Nje ya Jiji la Mbeya na itakua na urefu wa kilometa 48.9.
Ndege za
@AirTanzania
kwa sasa zinatoa huduma katika vituo vya ndani vipatavyo 15 ambavyo ni Mwanza, Bukoba, Songea, Zanzibar, Mtwara, Mpanda, Dar es Salaam, Iringa, Gita, Kigoma, Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, na Tabora.
Mwonekano wa barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu yenye urefu wa km 260 sehemu ya Tanzania na Rumonge-Gitaza yenye urefu wa km 45 sehemu ya Burundi ambayo ni sehemu ya mtandao wa barabara za Afrika Mashariki itakavyokuwa.
Muonekano wa Meli mpya ya MV Mwanza"Hapa Kazi Tu" inayojengwa Kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bil. 109 na kampuni za Gas Enter Ship- Building Engineering na Lang Nam Corporation za nchini Korea, inayotarajiwa kushushwa kwenye maji February 12, 2023. Jijini Mwanza.
📍Kigoma
Muonekano wa barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu yenye urefu wa kilometa 260.6 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami unaendelea mkoani Kigoma.
Rubani Neema Swai wa
@AirTanzania
ndiye anarusha BOEING 767-300F AIR TANZANIA CARGO toka Marekani hadi Tanzania tayari yuko angani kuelekea JK Nyerere International Airport muda wa kuwasili kuanzia saa nane mchana.
Kiwanja cha Ndege cha Moshi.
•Kuboreshwa barabara 2 za kuruka na kutua ndege, ya 1 mita 1,240 (Lami) na ya 2 yenye urefu wa mita 1,350 (Changarawe).
•barabara 2 za mchepuko ya ndege (Taxiway),
•barabara ya kuingia na kutoka kiwanjani na uzio.
•maegesho ya ndege.
Rubani Neema Swai wa
@AirTanzania
tayari amewasilia na BOEING 767-300F AIR TANZANIA CARGO toka Marekani katika JK Nyerere International Airport jijini Dar es Salaam.
Daraja jipya la Wami,
Urefu wa mita 513.5, upana mita 11.85
barabara unganishi km 3.8 linaunganisha mkoa wa Pwani na Tanga, litachochea ustawi wa jamii kiuchumi na kuleta maendeleo kwa mikoa ya kaskazini mwa Tanzania.
Waziri
@MbarawaM
apokea Ndege ya Shirika la Ndege la Air France aina ya Boeing 787-9 ambalo kwa mara ya kwanza toka kuanzishwa kwake, imetua katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
#KaziKazi
Muonekano wa hatua za ujenzi wa Daraja Jipya la Wami litakalokuwa na urefu wa mita 510 na upana wa mita 11.85 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa kilomita 3.8 ukiendelea mkoani Pwani.
📍Kigoma.
Muonekano wa Barabara ya Kibondo- Mabamba yenye urefu wa KM 47.9 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami utaanza rasmi baada ya kusaini Mkataba wa Ujenzi na Kampuni ya Chico kufanyika leo.
Barabara hiyo inaunganisha mkoa wa Kigoma na Kagera, Geita na nchi ya Burundi
MV MBEYA II
Meli yenye uwezo wa kubeba abiria 200 na mzigo wa tani takribani 200 yakamilika na kuingia ziwa Nyasa
Meli hiyo Itakuwa ikifanya safari zake katika Ziwa Nyasa kwenye bandari mbalimbali zilizoko upande wa Tanzania, kueleka Msumbiji na Malawi.
Moja ya mitambo mipya ya kushusha na kupakia makasha ukiwa katika hatua za mwisho kufungwa katika Bandari ya mtwara utakaokuwa na uwezo wa kuhudumia makasha 35 Kwa saa, mradi huo unatarajiwa kukamilika na kuanza kazi mwishoni mwa mwezi march 2023.