Joramu Nkumbi Profile Banner
Joramu Nkumbi Profile
Joramu Nkumbi

@NkumbiJoram

Followers
53,094
Following
334
Media
1,339
Statuses
2,368

Author 6 Books AMAZON 📚📚=| MBA | MLUMBI I Leadership Expert /John 15:16 IMC | Trainer-0757464874 MD:AYLF and PLO Lumumba Foundation SUB YOUTUBE —Joramu Nkumbi

Tanzania, East Africa
Joined June 2014
Don't wanna be here? Send us removal request.
Explore trending content on Musk Viewer
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Siku Saba Zilizopita 1.Leo 2.Jana 3.Juzi 4.Majuzi 5.Juzijuzi 6.Majuzi yale 7.Kijomba. Siku Saba Zijazo 1.Leo 2.Kesho 3.Keshokutwa 4.Mtondo 5.Mtondogoo 6.Kitondo 7. Kitondojogoo au (kitojo)
Tweet media one
216
657
4K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ni kicheko taanusi mhadhiri anapopata sabatiko, ni kicheko bojobojo mwana anapoona titi la nina, ni kicheko tumbitumbi baharia anapopata halasa, ni kicheko belele mkulima anapopata mtamba na liweya, ni kicheko biwibiwi biharusi anapopata ukonavi, wewe kijulanga unachekea nini?
Tweet media one
354
321
4K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Uzimbezimbe na uzohali mshahara wake ni ukata, msaragambo na mtulinga malipo yake ni ukwasi, magamaga na kuwa fumbwe mshahara wake ni sekeneko, Usalata na ufyosi malipo yake ni gunia la aibu na fedheha. Bali jamala na insafu malipo yake paradiso. Ewe mja nadhari njia ya peponi
Tweet media one
197
174
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Ulumbi Kila pahala, kwa Makadara yake Mola nipo na Profesa PLO Lumumba - Bungeni Tanzania
Tweet media one
46
83
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Janja janjaruka, wakahambarara walipoulizwa wakaona kimuyemuye. Wakajaribu kupiga mafamba na kunyenga kwa nyama ya ulimi ila hawakufanikiwa kwa busara za wanakijiji. Hatimaye wakatema cheche kandokando ya balasi la petroli ndiposa amani ikatoweshwa, nayeyuka.
Tweet media one
130
100
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Uso kwa Uso na Prof. PLO LUMUMBA wa Kenya 🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪
118
200
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
- Naomba ushauri wowote wa maisha -
Tweet media one
409
52
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
6 months
Happy Birthday to Me Leo ni siku yangu ya kuzaliwa, Niombee kwa Mola 🙏🙏🙏
Tweet media one
296
121
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Nipo Katika Chuo Kikuu cha Syracuse mahali ambapo Rais wa Marekani JOE BIDEN alipata Shahada yake ya Sheria. Na Katika chuo hiki ndipo alipompata mkewe Neilia Hunter na kumuoa.
Tweet media one
160
55
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Mimi mja chochole nilipokutana na msharafu ONI SIGALLA alinifunulia gombo na kunipa waadhi nishikilie kidinindi, ama kwa hakika maneno ya mswahili ni kikoi cha kibiri hayachakai. Ukarimu wake ulinirovya rovurovu kama biskuti ndani ya kiowevu. Akraba yangu shukrani belele nayeyuka
Tweet media one
120
89
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kwa Neema za Mwenyezi Mungu jaalia, nimefika Salama- 🇺🇸🇺🇸🇺🇸✈️🇺🇸🇺🇸 Mwana mtembea kule huwakaribia wazee wa kale. Ulumbi popote
Tweet media one
62
61
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kwa maneno dhahiri shahiri,Mama amtemea mgogoyo mwanake kigoli. Ewe banati mwenye pambo la bronki na bizimu na tabasamu taanusi chunga maago wana miba nungunungu.Mama alipomaliza kutema mgogoyo alikema, ayala mwenda pweke ni tijara ya mwindaji.
Tweet media one
162
86
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ulumbi popote
Tweet media one
37
41
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
4 months
“SAKO kwa BAKO”
Tweet media one
103
53
2K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Anza kusema, Kiswahili ni lugha AKRAMA.
62
141
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ya Upenuni nayaweka hadharani
84
173
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Msharafu SALIM KIKEKE @Salym - ilikuwa ni TAJAMALA kuonana Ushauri wangu kwa mja, endelea kuwa Upande wa Mola, “MEZA MRUTUTU”dhiki yako ni ya Kitambo, heshimu Wazazi na tambua kwamba mwana mdharau nina atakula MUMBI, mwana mdharau ibada kuzimu enda Kiona. Nayeyuka 🙏
Tweet media one
107
82
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ndugu zangu Waswahili, mwenye nguvu mpishe- Mimi ni kingulima, tena kishirazi, tena kidurusi huwezi nifananisha na mlima Kilimanjaro huko ni kunionea bure bilashi Mswahili Madebe apewe heshima yake 🙏
Tweet media one
77
50
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Safari ya Ulumbi, Uso kwa Uso na Sky, Ndugu wa Simulizi na Sauti.
46
124
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kuza Ulumbi 1. Hawala = Cheque 2. Wasifu Kazi = CV 3. Sodo/mlembe = Sanitary Pad 4. Mwago = Send off 5. Kisengeretua = Remote 6. Kikuta = Round about 7. Kikutashoto = Keep left
Tweet media one
119
218
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
8 months
Give a man land, give a man a wife, and don't tell him anything; he will stay there forever. I came, I saw, I loved. To the beautiful people of Rwanda, Africa is one.
Tweet media one
96
72
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ndugu, kula ugali wako kwa amani, salimia majirani zako kwa furaha, ota jua, kunywa maji ya kutosha, kula embe, chungwa, mabokwe, ama karakara ikiwa una senti, patana na Mola wako, fanya jambo unaweza usinyoshe kidole. Safisha chumba chako kabla hujasafisha dunia. Nayeyuka 🙏
Tweet media one
53
130
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Leo kwa kudra za JAALIA,kwa kadari yake MOLA nimetembelewa nyumbani na TBC kufahamu zaidi ni nini hasa sababu ya safari hii ya ULUMBI. Kuja kuniona mimi kumenirovya rovurovu na kunitebweresha tebwere,napokea mambo haya kwa kuduwazwa,kwa DUA na SALA.Nayeyuka kwa tafakari za uketo
Tweet media one
85
84
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Amejawa HASANATI, Ingawa yeye ni Mti Mkubwa wenye mizizi na matawi yake kotekote ila ulikuwa radhi kumhifadhi mwana wa nyuni, mwana wa nyuni akapata kivuli japo kwa sekunde. Umejawa hasanati na huo ni uungwana mkubwa, shukrani belele akraba yangu janabi SALIM KIKEKE @Salym
54
115
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
29 days
Ubaya Ubwela - maana yake
47
215
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Hivi sasa Wadada nao wanapenda ULUMBI
Tweet media one
63
53
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
5 months
Ulumbi kila Pahala 1. Charger – kimemeshi 2. Appetizers –vihamuzi 3. Simcard – kadiwia/mkamimo 4. Memory card –kadi sakima 5. Business card – kadikazi 6. Microwave –tanuri ya miale 7. Cocktail party – tafrija mchapalo 8. Lift – kambarau 9. Toothpick – kimbaka 10. Scanner –mdaki
Tweet media one
102
188
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Enhe- TUNGA sentensi kwa kutumia angalau maneno mawili hapo Chini ?? Shindano limeanza …. 😂😂😂✅✅📚📚
Tweet media one
138
116
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Aina ya vilio
72
123
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Nikiwa karibu na Ikulu ya Marekani nilipata kuona msafara wa Rais Joe Biden
88
50
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Majibu ya Walumbi , yamenishangaza sana , 😂
Tweet media one
47
23
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kwa Makadara yake Jaalia nipo ndani ya Ukumbi wa Umoja wa Mataifa. Hapa ndimo Viongozi wa Ulimwengu hukutania. Hiki ni kiti chetu Watanzania, Kila ikifika Usiku huwa navua mavazi yangu ya kitumwa na kuvaa mavazi yangu ya kidiplomasia.Fikra hii siwezi kunyang’anywa.
Tweet media one
43
41
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Alipowaza kwa uketo aliitwa punguani,alipowaza kimyakimya aliitwa hamnazo, sasa anawaza jahara anaitwa mwendawazimu. kuishi ni kuchagua mzigo faafu wa kuhangaika nao.
Tweet media one
51
63
971
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
10 days
Msitu bila miche michanga ni Msitu mfu, “Chinua Achebe” aliwahi kuuliza Swali iko wapi miche michanga itakayo chipukia? Baada ya ile migomba mizee kufariki? Dua yetu uwe Salama ndugu yetu hadi utakapoturudia 🙏
Tweet media one
28
319
1K
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
IKULU YA MAREKANI The White House is the official residence and workplace of the president of the US. It is in Washington, D.C, and has been the residence of every U.S. president since John Adams in 1800. The term "White House" is a metonym means president and his advisers.
Tweet media one
58
22
976
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Mwanahisabati aliyependa ulumbi kwa penzi la maki, kwa chata na tamwa anakwenda akitondoa utondozi, kwa kuterema anatamani cheo cha raia mwema.
41
99
941
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ukipata nafasi jaribu kuishi, Maisha ni hidaya Maisha ni tajamala Maisha ni azizi Je, wewe ni masikini hata ushindwe kununua hewa ? Uza hofu nunua tumaini Uza huzuni nunua furaha.
Tweet media one
51
98
955
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Karadha ya Mshahara = Salary Advance Malipo ya Ajari = Malipo ya Overtime Lugha ya Safihi = Lugha Chafu, Likizo ya Uraufu = Compassionate Leave, ( kwa kufiwa, kuugua) Tanzu = Tawi Hiba = Zawadi Bainifu = Outstanding (sifa njema za kipekee) Nimetondoa Utondozi.
Tweet media one
43
116
935
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Muhtaramu Job Ndugai tulikutana Nairobi Kenya katika tukio la National Prayer Breakfast alialikwa kuwakilisha nchi, nilialikwa kuwakilisha vijana. Katika Mazungumzo aliniambia, “ Usiache kupigania kile unachokiamini, tafuta kuwa bora kuliko jana, kesho yako ina matumaini”
Tweet media one
39
36
945
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
5 months
Ulumbi Kila Pahala - UN HEADQUARTERS- NEW YORK CITY 🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸
76
120
945
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Tunga Sentensi ndugu yangu 🌴🌴 1. Install = Sanidi 2. Uninstall = Sanidua 3. Computer virus = Mtaliga 4. Pointer = Kidosa 5. PowerPoint = Kinuru weo 6. Hardware = Maunzi ngumu 7. Software = Maunzi laini 8. Device = Kitumi 9. Scanner = Mdaki
Tweet media one
82
204
899
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Baada ya kubainiwa kuwa ni kitimbakwiri alipigwa kalamu, sasa amepatwa na jakamoyo.
Tweet media one
38
33
879
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ewe kijulanga, ujana ni nini ?
82
98
861
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Vizazi Sita (6) 1. Mtoto 2. Mjukuu 3. Kitukuu 4. Kitukutuku au Kilembwe 5. Kilembwekeza 6. Kinying'inya Je, utamuona kinying’inya ?
Tweet media one
57
87
839
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Nasaha za mswahili
50
88
838
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kwa KADARI yake Mola akupe baraka kazole. Akuepushe na balaa na beluwa. Waama katika mipango yako usiwe KAYUSA.
Tweet media one
28
24
784
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Sehemu ya Pili
27
69
789
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Pan Africanism - The new revolution, the revolution of Love
34
63
775
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kuwa Mlumbi , Jenga Umilisi wa kuzungumza
50
76
786
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Mwanzo wakati naanza kusoma falsafa,kusudi nijue namna ya kuendesha maisha haya mafupi, nilimsoma Budha,Mahatma,Dr. MLKj, James Alen,Nyerere, Mandela,Wangari,nk. nilivutiwa kiukweli na kuwafanya wanasihi wangu.Nilimposoma Bwana Yesu kuna namna siwezi eleza nimependa falsafa yake.
Tweet media one
34
32
788
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Punda na Bwana Mkubwa - Sehemu ya Kwanza
21
121
776
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Nakuletea mambo ya ndemi na mathathi, jadi njema na asili.
74
61
760
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Ametononoka tena amewanda tangu alipoacha ulanzi, chang’aa na mtukuru, haendi tena kwa majaka, Kazini amerudishwa anakula masurufu marupurupu na mukafaa, Waama nadhari njia ya peponi. Sio kitimbakwiri tena ni yeye na Mola wake, Sako kwa bako na familia yake. Ewe mja sarifu maisha
Tweet media one
49
39
776
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Bilionea Ali Mufuruki aliwahi kuniambia Ipo tabia ya wakubwa inayoitwa “hypocritical behaviour - kicking away the ladder" Kati ya mwaka 1776 na 1940, wanasiasa wengi wa Marekani walikuwa wafuasi wa sera za kulinda masoko na kutokuruhusu wawekezaji kutoka nje.
Tweet media one
22
82
776
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Matabaka 5 ya Waswahili Kiuchumi 1. Mabwanyenye- Matajiri kupindukia, miungudunia 2. Walala heri- kipato cha kati 3. Walala hai- Wana Chakula cha kutosha tu 4. Walala hoi/Makabwela- Maskini, Mshahara kijungujiko, 5. Mafukara/Hohehahe/hawinde /fakiri - maskini kupindukia
Tweet media one
44
109
746
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
TBC TAIFA - tukuze ulumbi
35
86
750
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
8 months
See you in Kigali - Rwanda friends
Tweet media one
49
26
730
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kumbe na huku nyumbani SINGIDA wanafuatilia ULUMBI - akraba zangu waliponiona nikipita mtaani wakiwa katika hali ya MTIMBWIRIKO , kwa tamwa tulifurahi kwelikweli
35
56
714
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Mzee Mchekeamwezi alipokutana na Mzee Nunaucheke alimwambia umeadimika kama kicheko jehanamu, na kama barafu ya kukaanga, naye akajibiwa nawe umeadimika kama mizizi ya mawe na kama maziwa ya kuku. Wakacheka sana na kupigana pambaja kisha wakaambatana kama mkia na kupe.
Tweet media one
38
64
706
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Yaa Rabi Stara, jambo hili ni kweli ama ufifi tu ?
Tweet media one
82
58
720
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Anatamani bereti ingawa yeye si jemadari. Nayeyuka.
46
78
697
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Tumia hii, kwa chata na tamwa …..
53
81
689
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Kama una taarifa zozote za YANGA naomba, pia kama upo BERLIN - Ujerumani tuonane.
Tweet media one
26
21
676
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Maisha yenyewe zawadi angalia kama bado uko nayo
42
67
654
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kwa Kudra za Mwenyezi Mungu nilipata nafasi ya kumtembelea Seneta wa jimbo la Arkansas John Boozman. Huyu ni moja wa wanasiasa makini sana katika Taifa la Marekani. John Boozman is the senior US senator from Arkansas, a seat he has held since 2011 A member of the Republican P.
Tweet media one
47
19
666
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
HAKUNA WINGI WA MANENO HAYA:- Kampuni = Sio makampuni Dawa = Sio Madawa Karatasi = Sio makaratasi Uhusiano = Sio mahusiano Ununuzi = Sio manunuzi Pacha = Sio Mapacha Udhaifu = Sio Madhaifu
79
137
643
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Jahazi la Ulumbi liende mbele daima
35
64
625
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
4 months
Na Jamaa Zangu maskani, nawaeleza Asili ya msemo, “SAKO kwa BAKO”
20
62
629
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Kuza ulumbi ndugu; tunga sentensi 1. Ndiposa = Ndipo sasa 2. Ndisi = Ndiyo sisi 3. Ndiwe = Ndiyo wewe 4. Ngole = Mtu Mwongo, Laghai 5. Hawafu = Mtu Mwoga
Tweet media one
88
62
618
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Uso kwa Uso na msharafu, janabi January MAKAMBA na Salim Kikeke @Salym
22
61
601
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 month
Kila la kheri
Tweet media one
20
111
622
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Maana ya semi nilizozitumia; Meza Mrututu = Kuvumilia Machungu au Maovu Kula Mumbi = Pata taabu au Shida Meza Joto lako = Tuliza hasira yako. Nina = Mama
Tweet media one
28
41
598
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Pamwe na Msharafu Balozi wa Tanzania Nchini Ujerumani Dkt Abdallah Possi, Nimepewa MLAHAKA mwema hapa Ubalozini - Berlin, tumezungumza mazuri kisha nikapata Sharubati ya Zabibu na Udohodoho ulikuwepo mezani. Ndugu hawa wamejawa hasanati na ukarimu furifuri. Shukrani belele.
Tweet media one
33
19
600
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
JITIE MOYO mwanakwetu Tumia Abra kuongeza UMILISI wako Tumia Satua kujikwamua kwenye Lindi la unyonge Penda mvuvumko wa Afrika kwamba unaweza kufanikiwa ukiwa nyumbani Penda uanamajumui kwamba Afrika ni moja na binadamu wote sawa Penda kufikiria uko huru, Afrika ni Kanzi.
Tweet media one
22
40
600
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Mentorship is more caught than taught. Na msharafu Professor PLO LUMUMBA
Tweet media one
12
15
600
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Shukrani belele TBC, shukrani jazila Waswahili wenzangu, shukrani tumbitumbi walumbi, nayeyuka
20
52
578
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Bahari ya ujinga na bahari ya elimu ipi ina uketo zaidi ?
36
54
571
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Nimetondoa utondozi, kimuyemuye, mafamba, nyenga, kizinda, balasi na wahaka.
37
66
562
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
😂😂 Waswahili wanachukua kadha, wanaacha kadha wa kadha. 😂😂
41
32
543
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
White House, DC Mujarabu nilipofika karibu na IKULU ya MAREKANI wimbo wa Taifa la Tanzania ulianza kuimbwa, Moyoni nilifahamu kwamba Mwalimu Nyerere aliwahi kuimbiwa Wimbo huu alipokaribishwa na Mwenyeji wake rais JF Kennedy- Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania 🙏🙏🙏
41
65
558
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Baada ya kupoteana miaka na mikaka mujarabu walipoonana walipigana pambaja, kwa furaha riboribo walikumbatiana papatupapatu. Wakakumbushana habari za mchwa na vingulima na habari za kumbikumbi na vidurusi ndiposa wakacheka kochokocho. Ungewaona ungefurahi pia, nayeyuka kihawinde.
Tweet media one
39
38
539
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Miaka na Mikaka, Furaha na Buraha…….
32
75
526
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
AYO TV na Joramu Nkumbi - Kimombo ni Silaha tuliyoipora kwenye uwanja wa mapambano.
21
100
540
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Yule fukara fuke mlangoni.
21
49
534
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Rajamu, Mtanziko, Mtule, Mhafidhina,
36
91
529
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Jaribu kutunga sentensi ??? 1. WWW = Wavuti Wa Walimwengu 2. Online = Mkondoni 3. Charting Group = Kundi sogozi 4. Touch Screen = Kiwamba gusa 5. Smart phone = Sikanu TUNGA sentensi ???
Tweet media one
62
78
532
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
7 months
Mlumbi ni lakabu yangu, basi Ulumbi kila pahala
22
78
536
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
IKULU YA UGANDA - kwa KADARI yake Mola ndani ya kitala cha mtawala,
31
47
515
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Mwanahabari mwenye JAHA na ULUWA @Salym . Jina AJUADI, jina jema ni bora kuliko marashi ya marhamu ya nardo, mwisho wa safari hii ni mwanzo wa safari nyingine, Asante kwa kutuonesha namna mwanahabari bora anapaswa kuwa mfano faafu.
Tweet media one
12
19
522
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 year
Ulumbi umenipa familia kubwa sana Kila mahali ninapokwenda, Huyu ni Mtanzania mwenzangu Berlin Ujerumani. Amekuja kunisalimu na hili ni Jambo kubwa. Asante Sana kaka
Tweet media one
11
6
519
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Tangazo la kale lina ladha yake, bwana wee 😂
Tweet media one
48
89
517
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Afisa masuuli, masurufu na maduhuli
25
48
505
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
SYRACUSE- NEW YORK Baridi kali sana -20
31
28
514
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Nachelea kusema hewala!, -Ujumbe umfikie Mwanazuoni @MabalaMakengeza
28
58
504
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
New York City- Times Square “Learn from yesterday, live for today, hope for tomorrow. The important thing is not to stop questioning.” “He who can no longer pause to wonder … his eyes are closed.” “A happy man is too satisfied with the present to dwell too much on the future.”
Tweet media one
24
24
512
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Waama yule mwafulani alipopata fedha aliendekeza ugobo na usafihi, akaukana ungumbaru na kukumbatia ushababi shikamoo kuzikataa, kazini yakazidi matukulele na kazi kuipoteza, nyumbani yakazidi makuruhu na ndoa kuipoteza.Sasa jitimai yamsulubu kawa ngalawa iliyokosa mrengu anazama
Tweet media one
60
33
513
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 month
Sheria njema huwaleta wanadamu karibu na Mola wao. Tena hulinda maskini. Sheria njema ni Msingi wa Uumbaji. Sheria imo ndani ya Uumbaji. Sheria njema ni Gundi inayoshikilia Ulimwengu pamoja. Kitu cha kwanza ambacho Mungu alimpa Musa kwa ajili ya kujenga taifa ni SHERIA.
Tweet media one
14
89
519
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
2 years
Si mtu wa majaka, kakataa uzohali na ajizi, kufanya kazi za mtulinga na msaragambo kumempa kutabahari na kutopea katika biashara. Sasa si ajabu kuona mahuruji ya rajamu yake huko Dubai na Ulaya. Vilevile anasheheneza magari kutoka ng’ambo, sina shaka yeye ni Reginald Mengi ajaye.
Tweet media one
26
24
495
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
1 month
Mazungumzo yangu na NGUGI WA THIONG’O Hii ni kama bahati, Nikiwa British Columbia Profesa Sultan Somjee aliniunganisha na Prof. Ngugi wa Thiong’o nikapata kumsabahi kwa Simu Waama Mwana mtambaa kule huwakaribia wazee kwa kale. 🙏🙏🙏
18
64
516
@NkumbiJoram
Joramu Nkumbi
5 months
Sehemu Ya PILI , Ulumbi Kila Pahala - UN HEADQUARTERS- NEW YORK CITY 🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸,
32
50
509