Official Twitter Page for Rai ya Jenerali Juzuu III, by Jenerali Ulimwengu.
Launch Date - 6 Aug| Tweets are my own personal opinions|
@jeneralionline
hacked
Juzi mimi na mke wangu tulienda kumpelekea baba mkwe wangu, Mzee Gaspar Marealle, nakala ya kitabu changu. Mzee Marealle alitimiza miaka 100 January hii.
Nimefuatilia hili la Msigwa, na napenda kumshauri aombe radhi kwa Free kama alivyoomba kwa Abdul, kisha aachane na kauli asizoweza kuthibitisha, ni hatari. Musiba yuko wapi? Mwanaharakati huru kapoteza nini: uanaharakati au uhuru? Free hataki hela bali ushike adabu tu, basi!
Ni kwa huzuni, natangaza kifo cha baba mkwe wangu. Mzee Gaspar Marealle alifariki tarehe 16 May usiku. Alikuwa na miaka 103.
@theGandhiStore
@UlimwenguJm
Mr Ali Mody Kibao has paid a terrible price for living in a country where everyone is a merchant and some of us are selling our souls. We are one big Faustian contract and soon the Devil will come to collect his dues. Don't run, stand and deliver your souls!
Rest in peace, Ali!
Hivi huyu Sugu aliyepigwa na polisi na kusafirishwa kama gunia la mihogo ni yule yule show yake ilibarikiwa na Samia miezi michache iliyopita, na hivi Samia ndiye huyo huyo polisi wake wamefanya hayo ya kumtesa Sugu kwa niaba yake? Audhubillah minas shaytanir rajiim! Tumeisha!
Maneno kuhusu kulishana sumu yamekuwa mengi nchini na hiyo si hali salama. Wanasiasa wanazidi kuisukuma nchi hii kuelekea kuzimu na tusipofanya hadhari tutafika huko. Sifa ya uwezo wa kiongozi ni pamoja na kuitambua hii kama hatari na kuikemea na kuiondosha. Itatumaliza!
Hebu,jamani,tuache kumpaka Rais wetu mafuta kwa mgongo wa chupa. Rais haleti pesa za maenddeleo. Hiyo ni kazi ya Bunge, msimdanganye Rais, naye aache kusikiliza upuuzi huo. Wanafiki wakubwa kesho utawasikia wakisema tulimwambia lakini hakusikia. Hamjisikii haya?
Wapo miongoni mwetu wahalifu wengi na watenda dhambi wa kila aina. Mara nyingi hushirikiana katika usasi wa Dinari ya Kaisari wakitumia madhabahu ya Memon. Wanaouza maji ya DAWASA wakidai yamebarikiwa ni pamoja na hao wengine, makuwadi wa Ibilisi rajiim, na sote tuseme Amina!
Kweli IGP anaamini jeshi lake linafanya kazi ya kupongeza? Aaangalia picha hiihii yetu au anayo yake binafsi? Picha ninayoiona ni ya nchi inayoendelea kusasambuka hasa katika medani ya usalama wa raia wake. Naomba aangalie tena picha ya nchi, ataona ninachokiona. Asione haya.
Tuachane na utamaduni wa rais kuteua watu asiowajua, na mara kwa mara kuwatengua kabla hata hajawaapisha. Nafasi zitangazwe, anayejiona anatosha aombe , wasailiwe wote walioomba na aliye bora apewe. Usaili ufanyike hadharani, wananchi wawajue vyema hao wote wanaotaka nafasi hizo
Waliomo madarakani wanaipaka matope nchi yetu na kuonajisi hadhi yake. Wanatutangaza kama watekaji na wauwaji,,wezi, waporaji na majambazi ndio wanaiendesha nchi ya Kambarage. Hawa ni watu haramu .
It is obvious we have become a police state with no legality or legitimacy and those in charge don't give a damn who knows it. They have cloaked themselves in a web of impunity and a Devil-may-care arrogance. They are taking us to he'll and we are paying the fare.
Makada wa chama-tawala walikuwa wamezoea kubebwa na ngivu za dola. Unafiki wa kisiasa ulitawala. Hali hiyo sasa imebadilika, na wanasiasa wote watalazimika kusimama kwa nguvu zao.
#socialcontract
#crucialconversations
Episode 2:
Masikini Rais Samia! Mbowe anaweza sasa kudai kesi future kwa sababu Rais amekwisha kumhukumu kupitia matamko yake katika mahojiano na Kikeke. Majuzi tu Rais Samia alisikika akisema eti 'rais hakosei'. Hapa kakosea pakubwa. Kwa utaratibu wa mahakama halisia, Freeman is a fee man!
Seven years ago a heinous crime was committed by someone whom the government doesn't want to reveal. Now our babysitters in London are trying to wash our diapers, and show us who the criminals are but I won't be surprised if our dumb governors just say we are a sovereign nation.
Tunaendelea na hicho kinachoitwa michezo ambacho kingetakiwa kiitwe kwa jina lake halisi, yaani KAMARI. Hakuna mtu aliyeweza kutajirika kwa KAMARI.Tuache kudanganywa na wajanja wachache wanaotajirika kupitia mgongo wetu . Acha kucheza KAMARI na iepuke kuliko UKOMA na UKIMWI!
It's shocking beyond words what the Tanzania police is doing! I know it's not the whole force that is rotten but what we witness is proof that the country is in trouble and needs to take action lest we become another Sierra Leone, Somalia or Chad. I swear we are in a bad way!
Vazi, siyo various, samahani. Hakuna vazi lolote duniani linaloitwa la taifa lililoundiwa tume. Hakuna! Kuwafanya Watanzania watumie muda wao kusaka vazi la taifa ni wild-goose chase na diversionary tactic ili wasahau mambo muhimu yaliyowashinda watawala. Tusipotezeane muda wetu.
Mapya yanaibuka kila uchao! Kukosekana kwa fikra za kisiasa na kuendesha utawala na siasa kwa hisia za siku hadi siku ndiyo mambo yanayotuonyesha sasa kwamba tunapeperushwa na upepo na hatujui tuendako. Mkuu wa mkoa Arusha katumwa na nani kufanya kazi ya JESUS kwa mavazi yale?
Eti Rais kawapatanisha wakulima na wafugaji kwa kuwafanya wapeane mikono. Hii ni komedi isiyo na uhalisia wowote katika hali halisi. Matatizo ya wakulima na WACHUNGAJI ni ya msingi mno na Serikali imekua ikiichezea nachi muda wote. Haya makurdi yataendelea kupigana!
Nimeona mahali TUME YA UCHAGUZI Inatakiwa iitwe TUME HURU. Ahsante sana! Tuongeze kidogo na MCHANA tuuite USIKU na USIKU uwe MCHANA. George Orwell anakusanya makuhani na waumini kila uchao na nguruwe wanapaka lipstick na wanageuka kuwa walimbwende! Short-cut metamorphosis.
Yesterday, July 10, I took a Bolt cab from Nyerere Airport to Mbezi Beach, close to Shoppers Plaza. To my utter dismay, the fare was Tshs 58 000, which I'd never been charged even by ordinary cabs. I protested but the driver told me it was due to high demand. I didn't get it.
Kadri tunavyozidi kuishi ndivyo tujitahidi kupunguza uongo tuliomezeshwa kwa muda mrefu sasa. Kwa mfano kuna ofisi inayoitwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni kweli tunaye mtu kama huyo, au tuliye naye ni Waziri Mkuu wa Tanganyika ru? Tufikiri kidogo, tutaona.
Kwa keeling inachosha kusikiliza kila dakika sifa kwa Rais Samia, kutoka kwa kila anayehojiwa redioni. Mama Dokta imekuwa ni wimbo kila pembe... kumsifu bila kikomo hadi inakifu. Hivi hatuoni tunamfanya aonekane kama Kim Il Sung ambaye yeye na uzao wake wamekuwa miungu?
Tukemee jitihada zote za kijinga za kufufua uchifu nchini wakati ulikwisha kufa na kuzikwa. Sababu za kuufuta zilikuwapo na zilielezwa sawasawa wakati huo na wala hazijaondoka. Sasa hawa wanaotaka kuurejesha wantumia mantiki ipi? Wakati mwingine tunachezea moto bila kujua Atari.
Loliondo, Loliondo, Loliondo...hivi ni kwa nini watawala wetu ni viziwi, vipofu na vichwamaji hadi wanapoondoka madarakani? Ni ulevi, ulafi au ulimbukeni unaowafanya waamini kwamba wao tu ndio wana akili na wananchi hawana la kuwaambia? Hii ni laana kubwa itakayotutesa siku moja
Maradhi mengi yametukuta., na mengi tunaweza kuyatibu iwapo tutafanyà juhudi za dhati. Mojawapo ni la lugha. Chukua matamshi ya maneno yenye R na L na maneno yenye H
. Watu wanasema 'Nyelele' au 'fulaa' bila haya. 'Ninaflai kuwa apa kusheleekea uulu wetu!
Huu ni ugonjwa mkubwa.
Ali Hassan Mwinyi atakumbukwa kwa ujenzi wa demokrasia kisiasa na kiuchumi ,ujio wa yama vya siasa mbadala, uchumi huria na upanuzi wa uhuru wa habari. Katika masuala haya hakuna mwingine katika wakuu wetu wote aliyafanya kama yeye. Mpole., mnyenyekevu.,mstahamilivu, muingwana.
The death of Angola's Jose Eduardo dos Santos marks the end of another great African thief. He came to power apparently reluctantly but soon became a kleptomaniac surpassing Mobutu in his appetites. Dour and pleasant. Jolly and charming. A sportsman and a fan of soccer. A thief.
Tumeona mikutano ya hadhara inafanyika bila fujo na watu wa hoja kwa utilivu. Huu ni ukomavu mkuu wa watu waliofungiwa kuongea kwa miaka 7 na bado wakajua kufanya uungwana wa kiwango hiki. Maana yake ni kwamba Magufuli ndiye aliyekuwa na fujo akilini mwake, si wapinzani.
Wanampaka MAFUTA KWA MGONGO WA CHUPA. Hawaamini hayo wayasemayo, wanajikomba, wanajipendekeza, hawana haya hata kidogo. Ni watu hatari. Samia hatakiwi kuwaamini, na kama atawaaminni atajikuta amekwama muda si mrefu. Ajizungushie wigo wa washauri mahiri wasiosita kumweleza ukweli.
Natumai Sheikh Alhad sasa atakuwa na wasaa wa kushusha pumzi, kutuliza akili na kuomba radhi kwa kufru aliyoitoa kuhusu utukufu aliomvika Magufuli kwa kujipendekeza na kutudhalilisha sote Waislamu na Wakristo. Sasa anao muda wa kujutia ujinga na kiwewe cha kipindi kile cha hovyo
Jamani, kuna mtu hataki/ kitu hakitaki kupunguza gharama ya maisha ya Watanzania; mtu huyo /kitu hicho hataki/hakitaki kuunganisha magari yetu na nishati ya gesi asilia. Naambiwa mtu huyo/kitu hicho ni wamiliki wa SHELI zinazoongeka kila siku wakati gesi ipo. Kulikoni?
Ningependa kushiriki mjadala wa Katiba, kuhusu masuala kadhaa ninayoyaona kuwa na muhimu mazito. Leo naanza na mdaraka ya rais, jambo ambalo limejadiliwa sana. Naunga mkono msimamo unaolenga kupunguza madaraka hayo, kwa sababu yanapunguza ushiriki wa wananchi katika maamuzi.
Iwapo tunataka kitu cha kututambulisha kama taifa tujadili mbinu za kutufanya watu wa kuchukia na kupambana na rushwa na uonevu. Tukivaa sare hivi tulivyo mavazi hayo yatakuwa utambulisho wa waongo, wala rushwa na walaghai. Tutafute kitu kingine cha kututambulisha duniani
Apropos of nothing at all, Queen Elizaeth ll left Kenya to become monarch at the very time the Mau Mau uprising was used by British officials to torture, rape and kill tens of Kenyans in what was termed the 'Pipeline'. She never once spoke a word of the crimes. Just remember
MASHIKOLO MAGENI! Hivyo ndivyo wangesema Wasukuma kwa kuangalia msukumo mzito uliowekwa nyuma ya bisshara ya BETTING. Ni kwa nini? Nadhani waendeshaji wamegundua sisi ni majuha na wahirikina tunaoamini tutaokota dodo chini ya mchongoma. Wametuelewa sisi na serikali yetu.
Baada ya kuwa shughuli za kisiasa zimefungiwa kwa ZAIDI YA MIAKA 6, sasa zimeanza tena kwa maelekezo ya Rais Samia. Mikutano ya hadhara imeanza na imeamsha uchangamfu mkubwa miongoni mwa washiriki nchini wote.
@CSLitigation
@Benson_Bagonza
@SheikhPonda
A whole stream of jokers, clowns, comedians, stuntmen and jugglers in all walks of life including politicians, clergy, varsity dons and intellectual acrobats.. singing the same songs of praise to the throne with no shame or pity to themselves,only pursuing the crumbs of bread
We are ruled over by jokers. Only we dont laugh. Because the jokes are in such bad taste even a clown would cry. These people are irredeemable in their stupidity and cluelessness.
Hivi kuna mtu anajiuliza maana ya kumwita Rais Hussein Ali Mwinyi "Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi"? Nini hasa shughuli za Baraza hill? Nauliza tu.
Njia moja ya kupunguza madaraka ya rais kupunguza sana nafasi za wakuu wanaoteuliwa na mkuu mmoja kama rais. Hawa ni wengi mno, na haiwezekani rais akawajua. Napendekeza inapotokea nafasi katika idara muhimu, itangazwe na watu wenye sofa waombe, wahojiwe hadharani,na waajiriwe.
PESA FASTA! PESA FASTA! PESA! FASTA! PESA FASTA! !PESA FASTA?? PESA FASTA?? PESA FASTA!! PESA FASTA!! PESA FASTA!! PESA FASTA!! PESA FASTA!! PESA FASTA!?PESA FASTA?? PESA FASTA!? PESA FASTA!! PESA FASTA!! PESA FASTA!? PESA FASTA?? PESA FASTA!! PESA FASTA!! PES.unaliwa fasta!
I love Donald trump's predictability. The Harris team want a debate rematch,saying it was a party and they want more. Trump says it's because HE won Taylor Swift endorses Kamala Harris and Trump responds he is no fan of hers. You can never beat Donald Trump. He is the bestest.
Waziri Damas Numbaro, usiwatishe watu kwa kuweka marufuku ya kuwapokea wapinzani wa Simba au Yanga . Wahawishi, wawe na haya, wafanye kama zifanyavyo nchi nyingine. Usitoe amri wala vitisho kuhusu hili, la sivyo tutafikia hali ya kupewa amri tufurahi au tupende au tuchukie!
Kuna tatizo limekaa mbele yetu linatutazama isoni lakini sisi tunajifanya hatulioni. Ili turejeshe siasa za ushindani inabidi serikali ieleze hizo siasa zilikuwa zimezuiliwa lini na nani. Nijuavyo mimi hakuna sheria ya Bunge wala tamko rami la zuio kama hilo. Ni matamko tu, basi.
Somo hili ni kwa wote mlio maofisini na mnadhani mna madaraka makubwa. Hamna lolote isipokuwa hiyo mirage of power, kivuli cha madaraka ambayo unaweza kukitumia kuiba, kubaka na kula hadi ukavimbiwa, lakini machoni mwa watambuzi, wewe utabakia kuwa mwizi, kibàka, mbwa-koko tu.
Bahati njema nimemsikia msemaji mkuu wa setikali Mobhare Matinyi akisema yale yanayosemwa kila siku bila maelezo ya martini. Matinyi atueleze hizo fedha anazotoa Rais kwenda kujenga hayo yote, anazitoa wapi? Nilidhani yeye ndiye angesaidia kunyoosha maambo, kumbe naye yumo !
More reports are coming to us of people getting knocked over by bodaboda cycles. If has to be stopped . We need to be able to walk on the pavements without being killed. Police have totally abdicated their responsibility and become passive onlookers. Someone help us please!
Kama vile homa za vipindi. Kila baada ya muda. Sukari huwa chungu. Kila mara tunabaika. Kila mara ni suala jipya. Kila mara waziri atajiuzuru. Kila mara tutarudia tena. Kila mara hatujajifunza. Kila mara.
@MariaSTsehai
Endelea, Maria, na hizo spana. Inabidi sasa kuongeza na funguo za kufungua masikio yaliyozibwa kusudi ili vyura wasisiikie. Bora kuweka kumbukumbu hizi ili wakija siku moja kuzinduka kutoka uziwi huu wa hiari wasidai hatukusema.
Waswahili walisema'Mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi'. Ndivyo walivyolelewa. Anayempinga rais apigwe, akamatwe, auliwe. Its deeply ingrained in the psyche of these people and they just can't help it. It has become religious and knee-jerk. Zero thinking and all reflex.
Celebrating 33 yrs with
@raiyajenerali
!Reflecting on our journey-a tapestry of love, laughter, shared struggles & the joy of raising beautiful children. Here's 2 the countless chapters we've written & the adventures yet to come. Cheers to a lifetime of love & cherished memories!
Edward Lowassa's passing is a very sad event in our country and its politics. He served with unmatched dedication and energy but was done in by circumstances he couldn't control. May his soul rest in peace and may his family find courage and fortitude in rhese sad times
Now Trump says he won't debate again. Does this mean something? Kamala says let's have some more but Trump says no more. The small lie has run its course and the big bully knows he's licked fair and square. No more, he says, the whole debates thing is rigged!
Huku kupanda kwa bei ya mafuta kunatukumbusha tena yale mambo mengi ambayo huwa tunayachukua kirahisi mno mpaka linapotokeza jambo la kutuzindua kutoka usingizini. Ni hivi: si kila wa kipato wastani kama mwajiriwa anaweza kumiliki na kuendesha gari binafsi. Gharama zake ni kuwa!
Kamala Harris' arrival in the US campaign circuit.has visibly rattled the Trump/Vance ticket and I suspect they will shoot themselves in the foot multiple times as they grapple at adjectives to smear Kamala and whomever she picks for VP. Stay tuned for fun and laughs.
Hakika ni vyema kutoa sifa zifaazo panapostahili. Ikikithiri inakuwa unafiki na kujikomba, kujipendekeza kwa kutaraji kitu toka kwa huyo tunayempaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Inachusha kwa mtu mwenye hisia za utu na heshima. Tupunguze angalau kidogo huu unafiki uliopitiliza.
Kwa keeling inachosha kusikiliza kila dakika sifa kwa Rais Samia, kutoka kwa kila anayehojiwa redioni. Mama Dokta imekuwa ni wimbo kila pembe... kumsifu bila kikomo hadi inakifu. Hivi hatuoni tunamfanya aonekane kama Kim Il Sung ambaye yeye na uzao wake wamekuwa miungu?
Tell me somebody, on what record did our Speaker run, what credit dies she have as a legislator in her country that she can be hoped to transfer onto the international stage? Or does it not matter what you have done nationally when you seek office outside your country?
@KKagasheki
Huyu ndiye yule tabibu alikataa UCHAWA kwa Magufuli kwa kuheshimu taaluma yake. Wengine ni waroboto hadi leo na uroboto umewaganda kama sumaku. Aibu kupoteza fedha ya nchi kuelimisha waroboto wasio na faida kwa Taifa lao wakati hiyo pesa tungewagawia ombaomba. Hongera Faustin!
Inabidi tujenge utamaduni wa kufikiria kila tunachoona na kuambiwa. Ni muhimu kujiuliza swali moja kuu, linaloitwa swali la Kisokrati, the Socratic Question, nalo ni, Kwa nini? Why? Kijerumani Varuum? Kifaransa Pourquois? Kihispania Porque? Hata Wahaya wanalo: Kubaki?
Vladimir Putin has finally eliminated his best known opponent and the world is powerless to do anything. It may have been pretty obvious that this young man was risking something as dark as this. But the duty of patriots sometimes makes them moving targets.
I've heard a lot said about the growing number of churches in our countries and the revesal of the trend in Europe. It is a question of the difference between superstition and enlightenment, between BELIEF in miracles and KNOWING they don't work . It's very simple, really.
Vijana wetu wanaotafuta kazi watumie mitandao kusaka fursa za ajira, biashara, ujuzi na taarifa ili kupanua upeo wao kwa kujiunganisha na ulimwengu mpana, siyo kujifunga katika umbeya, udaku, ubazazi, uzuzu na uzezeta na aina nyingine za udumavu wa akili. Turekebishane pamoja!
@ulimwegujm
.I join our children in wishing my darling wife Josephine a hearty Happy Birthday and many more returns of the same. I look forward to a life of continued love and happiness with wife, who has shown all around her the true meaning of love and friendship. 61 Cheers!
Njmemwona mzee mmoja wa jijini Mwanza ktk kipindi cha TBC kuh vijana wanaoenda Butiama. Mzee Hamisi anasimulia alivyomjua Mwalimu JK Nyerere miaka ya 1950 na jinsi wananchi walivyokuwa wakichanga senti 50 kumwezesha Mwalimu kwenda UNO. Siku hizi moyo huo uko wapi, mbona hatuuoni?
Once again Israel is confirmed by thr ICJ as a pariah state practising Apartheid against the Palestinians. Of course Israel will ignore this verdict because Washington, London, Paris etc will continue backing this illegality but international public opinion is so clear again.
Mzee Hamisi amenikumbusha mzee mmoja wa TANU wa njini Bukoba, Ali Migeyo, au Ali Migeyo Matata, mtu machachari kweli! Alikuwa na ujasiri wa kipekee kupambana na wakoloni na kuhimili vitendo vya kupigwa mabomu ya machozi nk. Hawa wamesahaulika kabisa siku hizi, siku za miyeyusho!