Miaka ya 90s mpaka 2000s Miziki ya Bongo Flava ilikuwa na Beats kali sana, Msinitenge ya Profesa Jay kwangu ndiyo Beat kali ya muda wote. Kwako ni Beat gani unaikubali mpaka kesho?
Sio kwa ubaya! Lakini kwanini Misaada hasa tunayopeleka kwa Watu wenye mazingira magumu isiwe Nafaka, Mafuta, sabuni, mavazi na vitu ka hivyo. Hizi juisi, soda sijui maji ya viwandani ni kweli ndicho wanachohitaji?.
Ukimkuta Bi mkubwa kama huyu barabarani jitahidi umuungishe tu, nunua hata kama sio mlaji wa hicho anachouza. Hawatafuti utajiri hawa bali wanatafuta mkate wa kula wao na watoto wao.
As salam Alaikum ndugu zangu katika imani, bila makasiriko wala chuki Muislamu ukiangalia watu wako wa shida na raha utagundua wengi ni Wakristo kuliko Waislamu. Unadhani tatizo ni nini hasa? 🤔
Hii ilikuwa bonge moja la ngoma na ilipendwa na watu wengi kutokana na ujumbe wake, kubwa zaidi ni ubinifu uliotumika ndani ya hii video. Kama unaikumbuka taja jina lake.
Miaka kadhaa nyuma kiwanda cha Bongo fleva kilikuwa na hiki chuma DULLAYO, moja kati ya mashine zake tata ni NAUMIA ROHO. Anyways sijui mwamba yuko wapi now ila nilitaka tu kusema Dullayo anajua sana 🤞🏼