Ukienda Gym hauwezi jenga misuli kwa kukiangalia tu chuma ila unajenga misuli kwa kunyanyua chuma , hata kwenye maisha pia unakomaa kiakili kwa kuzibeba changamoto zako mwenyewe sio kwa kuziangalia tu na kuzikwepa 😎 .
Pesa unatumia uku ukijua fika kua umebakiwa na kiasi gani lakini Muda ndio rasilimali pekee unayoitumia bila hata kujua kua imebaki kiasi gani , Hivyo tumia muda wako kwa uangalifu maana hujui muda wako utaisha baada ya muda gani 😎 .
Kitakacho kutofautisha na watu wengine sio uwezo wako wa kufikiri hapana , maana kila mtu anafikiri ila ni ujasiri wako wa kuamua lililo sahihi baada ya kufikiri na hapo ndipo huleta tofauti 😎 .
Kua makini na watu unaonyanduana nao , baadhi yao wameshalala na watu walioko kwenye vifungo vya kishetani kazi yao ni kusambazia watu nuksi na mikosi kwa njia ya ngono 😎 .
Wakati mwingine kua mpole sana nako kuna karibisha dharau , kupuuzwa na kupata malipo yako chini ya kiwango hivyo unatakiwa kujiamini , madaha kama yote , tawala mazingira yako na uwaruhusu wanao kuchukia wajisikie vibaya kwa tambo zako 😎 .
Usiogope fedheha ndogo ndogo za kuishi kimasikini kwa muda tu , ila Ogopa kuishi maisha yasiyo na Uhuru ndani yake na yenye kuongozwa kwa misingi ya uongo na usaliti 😎 .
Hakikisha siri zako na mipango yako unabaki nayo mwenyewe , maana uyo rafiki yako nae ana rafiki ake ambaye wanapatana Sana na ambae wewe sio rafiki yake ✍🏿 .
Laiti Kama ungelijua ni muda mfupi kiasi gani watu hutumia kumsahau marehemu , Basi ungeacha Mara moja kuishi ili kufurahisha watu wengine na ungeishi maisha yako 😎 .
Hakikisha haujidanganyi mwenyewe ila unamuabudu Mwenyezi Mungu katika roho na kweli na wala usidanganyike na miujiza maana hata waganga pia hufanya miujiza 😎 .
Kuna wengine usione mambo yao kwenye maisha yanaenda na kutokea chap chap ukaona wivu hapana,huenda muda wao pia ni mchache . Hivyo jifunze kuPenda maisha yako na wala usitamani maisha ya mtu 😎 .
Kua makini na aina ya watu ambao hawajawai kukupongeza ukifanya vizuri wala kukubaliana na kile una hokifanya ila wao wanapenda wawe wana kukosoa tu 🤔 .
Kadiri muda unazidi kwenda kwenye maisha yako utagundua kua maisha hayawi maraisi ila ni wewe ndio unatakiwa kuongeza nguvu na ufanisi ili kwenda nayo sawa 😎 .
Dunia sio tamu wala sio nzuri Kama ilivyopambwa na kutamanisha , Hivyo Tafuta sehemu wanako muabudu Mungu katika roho na kweli ufanye ibada kwa faida ya nafsi yako 😎 .
Kwa bahati mbaya Kama ilivyo kwako huwa umthamini mtu asie na faida kwako , kadharika wewe pia hutoheshimiwa wala kuthaminiwa na yeyote yule usie na faida kwake 😎 .
Kwa kawaida kila chenye mwanzo lazima kifike mwisho iwe mahusiano ya kindugu , kirafiki au kimapenzi habari njema ni kwamba maisha bado yanaendelea hata bila ndugu , rafiki au hata mpenzi 😎 .
Haimaanishi kwa sababu tu una kiu basi ndio unywe adi maji machafu hapana utaharisha , Usiruhusu upweke ukufanye urudiane na ndugu, mchumba ama rafiki asiyefaa 🤔 .